2014-12-15 15:49:31

Bwana Dragan Covic akutana na Papa Francisko mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 15 Desemba 2014 amekutana na kuzungumza na Bwana Dragan Covic, mwanachama kutoka Croatia katika jopo la Urais Bosnia na Erzegovina. Viongozi hawa baadaye wamezungumza pia na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti aliyekuwa Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Viongozi hawa wawili wamejadili kwa kina na mapana hali ya nchi hizi mbili na kwa namna ya pekee mchango wa Kanisa Katoliki katika mchakato wa maendeleo endelevu ya ujenzi wa nchi hii baada ya kukumbukwa na mafuriko mwaka 2013 yaliyosababisha hasara kubwa. Wameridhika na mahusiano mazuri kati ya pande hizi mbili; mafanikio na changamoto zilizopo katika utekelezaji wa Itifaki ya mwaka 2006, ambamo pamoja na mambo mengine Serikali na Kanisa vilitiliana sahihi ya kushirikiana kwa karibu zaidi kwa ajili ya mafao ya wengi. Mwishoni, viongozi hawa wamegusia masuala mbali mbali ya kikanda na kimataifa.







All the contents on this site are copyrighted ©.