Papa Francisko, Hongera kwa Daraja la Upadre!"Besi Dei" ni tarehe 17 Desemba!
Daraja Takatifu ni Sakramenti ambayo kwayo utume uliokabidhiwa na Kristo kwa mitume
wake huendelea kutekelezwa katika Kanisa hadi mwisho wa nyakati. Hii ni Sakramenti
ya huduma ya kitume ambayo ina ngazi kuu tatu: Uaskofu, Upadre na Ushemasi.
Baba
Mtakatifu Francisko anapojiandaa kuadhimisha Siku yake ya kuzaliwa hapo tarehe 17
Desemba, Jumamosi tarehe 13 Desemba 2014 amefanya kumbu kumbu ya siku ile alipopewa
Daraja Takatifu la Upadre tarehe 13 Desemba 1969 baada ya kuhitimu masomo na majiundo
yake ya Kikasisi, huko Argentina. Baba Mtakatifu katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii, anawaalika kuendelea kumwombea katika maisha na utume wake.
Kunako
mwezi Juni 1992 aliteuliwa na Mtakatifu Yohane Paulo II kuwa Askofu msaidizi wa Jimbo
kuu la Buenos Aires, Argentina. Kunako mwaka 1998 akateuliwa kuwa ni Askofu mkuu wa
Jimbo kuu la Buenos Aires. Na kunako mwaka 2001 akateuliwa na Mtakatifu Yohane Paulo
II kuwa Kardinali. Kunako tarehe 13 Machi 2013 akachaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki
kama Khalifa wa Mtakatifu Petro.