Wiki ya Kuombea Umoja wa Wakristo:" Nipe Maji Ninywe "
Maaskofu Katoliki Kenya wametoa ujumbe wao kwa Wakristo wote , kwa ajili ya Wiki ya
Sala ya kuombea Umoja wa Wakristo, ambalo kila mwaka inafanyika kuanzia tarehe 18-25
Januari. Kwa mwaka 2015, wiki hii, inaongozwa na kauli mbiu: “Nipe maji ninywe”(Yh4,7).
Mwenyekiti wa Tume ya Kiekumeni Kwa Baraza la Maaskofu Kenya, Askofu Peter Kairo,
akitoa ujumbe kwa niaba ya Baraza la Maaskofu Kenya anasema kwamba, Mada ya mwaka
huu ambayo imeegemea katika aya za Yesu kukutana na mwanamke Msamaria kisimani, ni
mwongozo katika juhudi zote za kiekumeni na himizo la kuishi kwa kutegemeana mmoja
kwa mwingine licha ya kuwa tofauti. Ni wito wa kujenga umoja na mshikamano na udugu
kati ya waamini.
Ujumbe unaendelea kueleza kuwa, aya hiyo ni wito wa kufanya
upya dhamana katika kushirikiana. Ni mwaliko wa Bwana kutoa maji kwa watu wote wanao
waendea kama wahitaji, wanaotaka kujua, kujadiliana na kukubaliana na kila mmoja kuishi
utume wa Kanisa. Wakiwa na uthabiti katika kutegemea Bwana , upendo wake una uwezo
wa kubadilisha yote , kama ilivyo kwa mtu mwenye kiu kunywa maji. Bwana ni chanzo
cha maji hai yenye kuzaa matunda ya umoja halisi, ambayo Waamini wote wana kiu hiyo
kwa muda mrefu.
Hivyo, Askofu Kairo, anakumbusha kuwa, mwaka huu, mwongozo
katika tafakari za Wiki la Maombi kwa ajili ya Umoja wa Wakristo, umeandaliwa na
Baraza la Kitaifa, linalounganisha Makanisa ya Kikristo ya Brazil, taifa lenye
dini nyingi za Kikristo lenye kukabiliwa na "uso changamoto nyingi za kutovumiliana
kati ya madhehebu, na lenye kuwa na kiwango cha juu cha ukatili dhidi ya wanawake
na watu wa asilia.
Askofu Kairo anahisi waamini wa Kristo Brazil kama ilivyo
pia katika mataifa mengine, katika wiki hili wazamishe tafakari za kina katika kiu
hii ya kuwa na umoja katika tofauti, kwa ajili ya kuishi kwa uhuru kikamilifu. Kuondoa
tabia za kutovumilia wengine badala yake iwe kuheshimu tofauti halali na kukuza mjadala
kwa ajili ya mema ya kawaida.
Askofu Peter Kairo pia ameligeukia taifa
lake la Kenya na kusema hakuna tofauti na Brazil. Wakristo Kenya pia wako mbele ya
changamoto hii uwepo wa “Ukristo unao nadiwa na kufungamana na utafutaji wa fedha,
ambao umeibua makundi ya ubabe, vurugu na ubabe usiokuwa na kiasi katika baadhi
ya maeneo. Hivyo, Ujumbe unakamilisha na wito kwamba, Wiki hili la Maombi kwa
ajili ya Umoja wa Wakristo, ni nafasi ya kushuhudia matunda mazuri ya neema ya Mungu,
katika kuwapokea na kuwakaribisha wengine kwa moyo mkunjufu licha ya kutofautiana,
na kutokuwa wakamilifu,bado Roho Mtakatifu anasukuma waamini katika maridhiano na
umoja ,“Nipe maji ninywe. “