Tatizo la ekolojia linagusa kanuni msingi za kimaadili
Majanga makubwa yanayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi ni changamoto ya kimaadili
inayohitaji mabadiliko makubwa ya kifikra, ili kuleta matokeo yanayofaa kwa kuwa na
mwelekeo mpya wa maisha. Vigezo vinavyowasaidia walaji kuchagua na kuweka mitindo
mipya katika maisha ni utafutaji wa ukweli, uzuri, wema na ushirikiano wa pamoja kwa
ajili ya mafao ya wote. Mitindo ya maisha haina budi kuwa na kiasi, ukadiri na nidhamu.
Mwanadamu
katika miaka ya hivi karibuni amekuwa ni chanzo kikuu cha uharibifu wa mazingira na
matokeo yake yanahatarisha ekolojia nzima, changamoto na mwaliko kwa Jumuiya ya Kimataifa
kushikamana kwa dhati katika mchakato unaopania kudhibiti majanga yanayotokana na
mabadiliko ya tabianchi, ili kuendeleza kazi ya uumbaji, ambayo mwanadamu amekabidhiwa
na Mwenyezi Mungu kwa ajili ya mafao yake kwa sasa na kwa kizazi kijacho.
Baba
Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitando ya kijamii anawakumbusha
kwamba, ekolojia ni jambo muhimu sana katika maisha na ustawi wa binadamu na kwamba,
linagusa kanuni maadili. Itakumbukwa kwamba, wafuasi wa Baba Mtakatifu kwenye akaunti
yake ya twitter wamefikia millioni kumi na sita!.