2014-12-08 13:15:28

Majilio ni kipindi cha matumaini! Papa asema.


Jumapili Baba Mtakatifu akihutubia mahujaji na wageni wapatao 50 elfu waliotoka pande mbalimbali za dunia, alikumbusha kwamba, Jumapili ya pili ya majilio, unaendelea kuwa wakati wa maajabu ya kushangaza, yenye kutuhamasisha na kutoa mwamko mpya katika matumaini ya kurudi kwa Kristo na kumbukumbu ya kuja kwake kihistoria.

Papa alieleza huku akilenga katika liturujia ya Neno kwa Siku hiyo, kwamba, mna ujumbe kwetu sote, ujumbe wa matumaini. Na alifanya rejea kutoka kitabu cha Isaya, aya zilizo zungumzia "Faraja , kwamba Mungu atawafariji watu wake. Papa alifafanua kwa kifupi juu ya aya hizo akisema zinahusu wakati wa furaha ya kukombolewa na wokovu, na wakati wa kutazama kwa matumaini siku za mbele kwa kujiamini

Papa alieleza na kusema, Isaya anarejea watu ambao walipita katika kipindi cha giza , lakini kwa sasa kwao wakati wa kufarijika umewadia, ambamo huzuni na hofu imegeuka kuwa furaha, kwa sababu Bwana mwenyewe anawaongoza watu wake katika njia ya ukombozi na wokovu.

Lakini, Papa pia alisisitiza na kuonya , haiwezekani mtu kuwa mjumbe wa faraja ya Mungu kama yeye mwenyewe hana uzoefu huo wa kuisha kwa kufarijiwa na kupendwa naye. Na ndivyo ilivyo elezwa katika somo la Injili, kwamba watu wanapaswa kulibeba neno la Mungu katika mikoba yao.Ujumbe wa faraja kutoka Somo la Isaya , unasikika tena Siku ya Jumapili hii ya pili ya Majilio, ni mafuta yenye kupoza uchungu katika vidonda vyetu wa kiroho, na kutupa motisha ya kufanya kwa bidii zaidi, katika kuiandaa njia ya Bwana.
Papa ametaja hali nyingi, zinazoweza onyesha faraja hii, lakini inahitaji kuwa ni ushuhuda wa kweli wa maisha ya muumini yenye kuishuhudia faraja hii, hasa kwa wale walioonewa na mateso, dhuluma na ukandamizaji, kuhusu wale ambao ni watumwa wa fedha, nguvu, mafanikio, na kuipenda dunia. Sisi wote tumeitwa kuwafariji ndugu zetu, kushuhudia kwamba Mungu tu anaweza kuondoa sababu za matukio ya kusikitisha katika yote kimwili na kiroho pia.
Papa alisema kwamba, ujumbe wa Nabii Isaya, unaendelea kuzungumza ndani ya mioyo yetu hata leo, kutuambia kwamba Mungu husamehe dhambi zetu na kutufariji kama sisi wenyewe tutamwendea kwa unyenyekevu na moyo wa majuto. Mungu, alisema Papa Francisko, amekwisha angusha chini kuta za uovu na kujaza mashimo ya uovu wetu, na kusawazisha matuta ya viburi na ubatili, na kusafisha njia ili tuweze kukutana pamoja naye, iwapo tutaridhia.








All the contents on this site are copyrighted ©.