Jifunzeni kutoka kwa B. Maria ujasiri wa kumwilisha Neno la Mungu!
Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican wanasema kwamba, kwa kusoma na kujifunza
Vitabu Vitakatifu, Neno la Bwana linaendelea kutukuzwa na hazina ya ufunuo ambayo
Mama Kanisa amekabidhiwa ijaze zaidi na zaidi mioyo ya waamini, hasa pale wanaposhiriki
kikamilifu katika Maadhimisho ya Fumbo la Ekaristi Takatifu, ili kukuza maisha ya
Kanisa pamoja na kuheshimu zaidi Neno la Mungu linalodumu milele.
Baba Mtakatifu
katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, tarehe 8 Desemba 2014, Mama
Kanisa anapoadhimisha Sherehe ya Bikira Maria kukingiwa dhambi ya asili, anawaalika
waamini kujifunza kutoka kwa Bikira Maria kuwa na ujasiri katika mchakato wa kulimwilisha
Neno la Mungu katika uhalisia wa maisha ya kila siku.