Mh. Padre Joseph Obanyi Sagwe ateuliwa na Papa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Kakamega,
Kenya!
Baba Mtakatifu Francisko ameridhia ombi lililotolewa na Askofu Philip Sulumeti wa
Jimbo Katoliki Kakamega kung'atuka kutoka madarakani kadiri ya Sheria za Kanisa namba
401ยง Ibara ya 1 na hapo hapo ameteua Mheshimiwa Padre Joseph Obanyi Sagwe, Paroko
wa Kanisa kuu na Makamu Askofu Jimbo Katoliki la Kisii, kuwa Askofu mpya wa Jimbo
Katoliki la Kakamega, nchini Kenya.
Askofu mteule Joseph Obanyi Sagwe alizaliwa
kunako mwaka 1967 huko Kebiro, Jimbo Katoliki la Kisii, Kenya. Baada ya masomo na
majiundo yake ya Kikasisi, akapadrsihwa tarahe 25 Oktoba 1996. Baada ya Upadrisho
alitekeleza utume wake kama Paroko msaidizi na Mratibu wa shughuli za kichungaji Jimboni
Kisii kuanzia mwaka 1996 hadi mwaka 1999.
Kuanzia mwaka 1999 hadi mwaka 2004,
alijiendeleza kwa masomo ya juu katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Laterani kilichoko
mjini Roma. Aliporejea Jimboni mwake kunako mwaka 2004 aliteuliwa kuwa Paroko wa Kanisa
kuu la Jimbo Katoliki Kisii na kuanzia Mwaka 2005 alikuwa ni Makamu Askofu Jimbo Katoliki
la Kisii, ambalo liko chini ya Jimbo kuu la Kisumu, Kenya.