Mshikamano wa upendo na wananchi wa Karamoja, Uganda
Imekwishagota takribani miaka 20 tangu alipofariki dunia Padre Vittorio Pastori, aliyefahamika
na wengi kama "Don Vittorione". Ni kiongozi aliyejitoa bila ya kujibakiza kwa ajili
ya ustawi na maendeleo ya wananchi wa Karamoja, walioko nchini Uganda.
Mara
baada ya Katekesi, Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 3 Desemba 2014 alipatiwa
zawadi na Chama cha Kitume cha Ushirikiano na Maendeleo Barani Afrika, kwa ajili ya
kuchimba kisima cha maji kitakachotumiwa na wananchi wa Karamoja, walioko nchini Uganda.
Chama hiki katika utume na maisha yake kwa kipindi cha miaka arobaini na tatu iliyopita,
kimeweza kuchimba visima vya maji elfu moja kwa ajili ya matumizi ya maji safi na
salama kwa wananchi wa eneo la Karamoja, nchini Uganda.
Katika tukio hili,
Baba Mtakatifu amemkumbuka Padre Vittorione kwa ushuhuda wake katika azma ya Uinjilishaji
wa kina unaogusa mahitaji ya mtu mzima: kiroho na kimwili.