2014-11-30 09:58:07

Watu 7, 000 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa Ebola


Taarifa ya Shirika la Afya Duniani, inaonesha kwamba, hadi kufikia tarehe 29 Novemba 2014, watu waliofariki kwa ugonjwa wa Ebola wamefikia 7, 000, wengi wao wakiwa ni wale wanaotoka katika nchi za Afrika Magharibi. Hadi sasa WHO haijatoa maelezo ya kina kuhusiana na kuongezeka kwa idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na ugonjwa Ebola.

Zaidi ya watu 16, 000 wamepimwa na kukutwa wakiwa wameambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola, tangu ulipofumuka huko Guinea, mwezi Machi, 2014. Guinea, Sierra Leone na Liberia ndizo nchi ambazo kwa sasa zimeathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na kuenea kwa ugonjwa wa Ebola.







All the contents on this site are copyrighted ©.