2014-11-30 16:28:20

Papa Francisko asema ziara yake Uturuki ni neema katika majadiliano ya kiekumene


Baba Mtakatifu Francisko, katika siku ya tatu na ya mwisho, ya ziara yake Uturuki, kati ya mengine, alishiriki katika katika Ibada Takatifu iliyofanyika ndani ya Kanisa Kuu la Kiekumeni la mjini Istanbul, kwa ajili ya Maadhimsho ya Siku Kuu ya Mtaktifu Andrea, kwa mujibu wa Liturujia ya Kanisa la Kiotodosi. Sikukuu ya Mtakatifu Andrea huheshimiwa kama mwanzilishi wa Kanisa katika Kiotodosi duniani. Liturujia ya kanisa hili ni ya zamani.

Papa Francisko, akihutubia kwenye Ibada hii alimshukuru Mungu kwa neema hii iliyomkutanisha na kiongozi wa kanisa la Kiotodosi, na kukutana kwao uso kwa uso, kubadilishana mawazo kukumbatia kwa amani, na kuomba kwa ajili ya umoja ni hatua muhimu katika safari ya kanisa, kurejesha usharika kamili wa wafuasi wa Kristo. Na kwamba taratibu zote hizi , daima zinapaswa kuambatana na mazungumzo ya kiteolojia. Mazungumzo halisi ya kina, si kukutanisha mawazo tu lakini kutazama katika ukweli wa Injili.

Baba Mtakatifu ameendelea kusema kwamba, amekutana na Kiongozi wa Kanisa la Kiotodosi kwa njia hii ya maridhiano na amani kati ya Wakatoliki na Orthodox , si kama ni jambo alilolizua tu kujuuju lakini msingi wake ni hamu ya tangu miaka hamsini iliyopita, waliyokuwa nayo watangulizi wao, Patriaki wa Kiekumeni Athenagoras na Papa Paulo VI, waliopokutana miaka hamsini iliyopita Yerusalemu.
Na kwa furaha, ziara yake imekwenda sambamba na maadhimisho ya kumbukumbu ya kupita miaka hamsini tangu azimio la Umoja wa Wakristo” Unitatis Redintegratio,”kupitishwa katika Maazimio ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, juu ya Umoja wa Kikristo. Hati hiyo ni msingi uliofungua njia mpya kwa ajili ya makutano ya Wakatoliki na ndugu zao wa Makanisa mengine na jumuiya za kikanisa.
Papa pamoja na kuzungumzia umoja wa Wakristo, pia alirejea katika hali za maisha ya kawaida ndani ya jamii, akionyesha kujali kilio cha watu wengi, wanaougumia kwa matatizo ya ukosefu wa mahitaji msingi si vitu tu lakini pia ukosefu wa usawa na uganadmizwaji wa haki zao msingi. Papa amesema, Kanisa haliwezi kupuuza juhudi za pamoja za kutoa utambulisho a nguvu kama wafuasi wa Bwana mmoja Yesu Kristo, katika kuwahudumia wahitaji na wanyonge. Watu maskini wanaopaza sauti wakiombe msaada. Sauti za watu maskini wake kwa waume, ambao ni wengi mno. Wale wanaokabiliwa na utapiamlo mkali, kuongezeka ukosefu wa ajira, kuongezeka kwa idadi ya vijana wasio na ajira, na kuongeza kutengwa na jamii.

Papa ametahadharisha kwamba, matatizo haya yanaweza kuwa kati ya sababu kubwa za kuongezeka kwa matendo ya kigaidi na uhalifu mwingine. Kanisa haliwezi kujificha au kuwa tofauti na kilio cha ndugu hawa, Hatuna jingine Kanisa linaloweza kufanya zaidi ya kuhimiza nyezo ya uadilifu, upendo na fadhila, kama silaha kuu katika kufanikisha mazingira ya kuokoa wengi - lakini juu ya yote, msaada wa kutetea hadhi yao kama binadamu, ili waweze kupata nguvu ya kiroho, na kwa mara nyingine, watu hao waone kuwa wao pia ni wahusika wakuu wa maisha yao wenyewe.

Papa aliendelea kuzungumzia jinsi ya kupambana na hali hizo katika mwanga wa Injili, hasa katika kuona sababu za miundo inayoleta umaskini, na ukosefu wa usawa, uhaba wa kazi ya heshima na makazi, na kunyimwa haki zao kama wanachama wa jamii na kama wafanyakazi. Amesema, Wakristo tumeitwa pamoja kuondokana na utandawazi wa kutojali wengine. Huu ni wakati wa kujenga kujenga ustaarabu mpya wa upendo na mshikamano.

Papa ametaja waathirika wa migogoro katika sehemu nyingi za dunia, inayosikika, akirejea kilicho tokea Ijumaa katika Msikiti wa Kano, Nigeria ambako watu zaidi ya mia wamepoteza maisha katika shambulio la kigaidi lisilokuwa na maana. Papaanasema matendo kama haya hayawezi kukubalika hasa pale mauaji yanayo fanywa kwa watu dhaifu na wasioweza kujitetea. Ameitaja kuwa ni dhambi na inaonyesha kiburi dhidi ya Mungu. Matendo kama haya, ni dharau kwa utu na heshima ya mtu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.
Papa alikamilisha maelezo yake kwa kurejea tena katika njia ya kutembea kwa umoja na mshikamano , akiomba Msaada wa Mtume Petro na Andrea nduguye kama walivyoomba watangulizi wa makanisa haya mawili, waanzilishi wa Makanisa ya Constantinople na Kanisa la Roma. "Tunaomba Mungu kwa ajili ya zawadi kubwa ya umoja kamili, na uwezo wa kukubali amani na utulivu katika maisha yetu. Hebu kamwe tusisahau kuomba kwa ajili ya mtu mwingine".









All the contents on this site are copyrighted ©.