2014-11-30 16:40:38

Papa aweka saini tamko la pamoja


Papa Francisko Kiongoza wa Kanisa Katoliki la Ulimwengu na Patriaki Bartholomew I, Kiongozi wa kiroho wa dunia ya Waothodosi, Jumapili hii, 30 Novemba, nyakati za mchana, waliweka sahihi zao katika hati ya Azimio la Pamoja kuonyesha hamu yao, katika kushinda na kuondokana na vikwazo, vinavyotenganisha Makanisa yao mawili. Aidha katika tamko hili, Viongozi hao wawili pia, wamelalamikia hali mbaya inayowakabili Wakristo na wote wanaoteseka kwa sababu ya imani au itikadi yao katika kanda ya Mashariki ya Kati. Azimio la viongozi hawa, linaihimiza jumuiya ya kimataifa kutoa hasa jibu sahihi, kwa ajili ya kikomesha mateso na mahangaiko ya watu yanayosababisha na binadamu

Maelezo yao yameonyesha kujali hali zinazoendelea sasa Iraq, Syria na Mashariki ya Kati. Kwa pamoja wanapenda kuona amani na utulivu vinarejeshwa katika mkoa huo na watu kuwa na mapenzi ya kukuza utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzo na maridhiano. Na pia wameonyesha kutambua na kushukuru juhudi zinafanyika katika kutoa msaada kwa kanda hii , na wakati huo huo, kutoa wito wao kwa wanaohusika wote, kubeba jukumu kwa ajili ya hatima ya watu, waweze kuimarisha dhamira yao juu ya jamii inayoteseka, na kuwawezesha, wanaoteswa kwa sababu ya imani yao kwa Kristo, hasa wale wote, walioamua kubaki katika nchi yao ya asili.

Tamko linasema , hawawezi kukata tamaa au kujiuzulu katika kuwatetea Wakristo wa Mashariki ya Kati ambao wamekiri jina la Yesu kwa kipindi cha miaka elfu mbili. Wengi wa ndugu hawa sasa wanateswa kulazimishwa kwa ukali kutoka makazi yao. Mahali ambapo hata thamani ya maisha ya binadamu inapuuzwa na kupotezwa bure. Hali hii inasikitisha hasa kwa wengi kutojali hali hiyo.

Tamko linaendelea kueleza kuwa , changamoto zinazokabili dunia katika hali ya sasa zinahitaji mshikamano wa watu wote wenye mapenzi mema. Kuona umuhimu wa kukuza mjadala wa kujenga umoja, kati ya Ukristo na Uislamu kwa misingi ya kuheshimiana na urafiki. Waislamu na Wakristo wameitwa kufanya kazi pamoja kwa ajili ya haki, amani na heshima kwa utu na haki za kila mtu, hasa Wale katika mikoa ambako waliwahi kuishi kwa karne nyingi katika mshikamano amani, lakini sasa na sasa wanapambana na maisha ya mateso na vita. Kama viongozi wa Kikristo, wanatoa wito kwa viongozi wa dini zote, wajenge hamu ya kuimarisha mazungumzo kati ya dini, kufanya kila juhudi kujenga utamaduni wa amani na mshikamano kati ya waaamini na kati ya watu.


Azimio hilo limefungwa na ombi "Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na katika kila njia. Bwana na awe pamoja nanyi nyote "(2 Thes 3:16).









All the contents on this site are copyrighted ©.