2014-11-23 11:45:26

Serikali ya mpito Burkina Faso yaanza kazi kwa makeke!


Rais Michel Kafando wa Burkina Faso na Luteni Kanali Isaac Zida, Waziri mkuu wameanza kutekeleza dhamana ya kuliongoza Taifa katika kipindi cha mpito, kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba 2015, kwa kula kiapo cha utii, Ijumaa, tarehe 22 Novemba 2014. Viongozi hawa wamefikisha kikomo cha uongozi wa Rais Blaise Compaorè alitebwaga mwanyanga hivi karibuni kwa kuhofia nguvu ya umma baada ya jaribio la kutaka kupindisha Katiba ya nchi ili aendelee kubaki madarakani kushindikana.

Rais Kafando kwa miaka kumi na mitano amekuwa ni Mwakilishi wa kudumu wa Burkina Faso kwenye Umoja wa Mataifa na amewahi pia kuwa ni Waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa. Katika hotuba yake mara baada ya kuapishwa Rais Kafando ameahidi kuanza mchakato wa kukomesha rushwa na ufisadi wa mali ya umma, ili kuhakikisha kwamba, haki inatendeka pamoja na kuwa n auhakika wa mahali ambapo Rais Thomas Sankara, aliyejitwalia madaraka kunako mwaka 1983 na baadaye kupinduliwa na Bwana Blaise Compaorè, aliyekuwa rafiki yake wa karibu mwaka mmoja baadaye.

Bwana Compaorè kwa sasa amekimbilia uhamishoni huko Morocco baada ya kuondoka Pwani ya Pembe ambako anashutumiwa kujihusisha katika machafuko yaliyojitokeza nchini humo hivi karibuni.







All the contents on this site are copyrighted ©.