2014-11-17 15:00:30

Balozi Mehmet Paçaci kutoka Uturuki awasilisha hati za utambulisho mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 17 Novemba 2014 amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Bwana Mehmet Paçaci, Balozi mpya wa Uturuki mjini Vatican. Hili ni tukio muhimu sana la kihistoria wakati huu Baba Mtakatifu anapojiandaa kufanya hija ya kiekumene nchini Uturuki.

Balozi Paçaci alizaliwa kunako tarehe 11 Septemba 1959 ameoa na ana watoto watatu. Baada ya masomo yake kwenye Chuo Kikuu cha Ankara kunako mwaka 1989 akatunukiwa Shahada ya Uzamili katika masomo ya kitaalimungu. Alifaulu kuendelea kufundisha Chuoni hapo kuanzia mwaka 1992 hadi mwaka 2008. Amewahi kuwa ni mshauri katika masuala ya kidini na huduma za kijamii, katika Ubalozi wa Uturuki, mjini Washington DC.

Kuanzia mwaka 2011 alikuwa ni mkurugenzi mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa katika Ofisi ya rais inayoshughulikia masuala ya kidini. Ni mtaalam wa lugha ya Kiarabu na Kiingereza.







All the contents on this site are copyrighted ©.