2014-11-14 14:19:39

Rais Tasso wa Perù akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 14 Novemba 2014 amekutana na kuzungumza na Rais Ollanta Moises Humala Tasso wa Perù na ujumbe wake waliomtembelea mjini Vatican. Baadaye, Rais Tasso amekutana na kuzungumza na Askofu mkuu Dominique Mamberti, aliyekuwa Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican, bila uwepo wa Kardinali Pietro Parolin ambaye kwa sasa yuko nje ya Vatican kikazi.

Viongozi hawa wawili wamesifu mahusiano mema kati ya Vatican na Perù na kwa namna ya pekee kabisa, kuhusiana na mchango wa Wakristo katika mchakato wa majiundo ya wananchi wa Perù bila kusahau mchango wa Kanisa katika ustawi na maendeleo ya wengi nchini humo katika kukuza na kudumisha utu na heshima ya binadamu; katika masuala ya kitamaduni na maendeleo ya watu.

Baba Mtakatifu na mgeni wake walibadilishana mawazo kuhusiana na masuala ya kisiasa na kijamii yanayojiri katika Kanda hii, kwa kujikita zaidi katika vichocheo vya maendeleo ya mtu mzima sanjari na utunzaji bora wa mazingira.







All the contents on this site are copyrighted ©.