2014-11-14 10:21:52

Jubilee ya miaka 25 tangu Agnese wa Bohemia alipotangazwa kuwa Mtakatifu


Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican kuanzia tarehe 13 hadi tarehe 16 Novemba 2014 anafanya hija ya kichungaji nchini Prague, kama sehemu ya maadhimisho ya Jubilee ya miaka 25 tangu Agnese wa Bohemia, alipotangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa Mtakatifu, tukio lililofanyika tarehe 12 Novemba 1989.

Tarehe 16 Novemba, wananchi wa Prague wanakumbuka siku ambayo siasa za Kikomunisti zilipobwagwa chini na nchi ikaanza mchakato wa demokrasia. Akiwa nchini humo, Kardinali Parolin anakutana na viongozi mbali mbali. Kilele cha ziara yake ya kikazi ni Jumamosi, tarehe 15 Novemba 2014, kwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu, kwa heshima ya Mtakatifu Agnese, Ibada itakayofanyika kwenye Kanisa kuu Mtakatifu Vito.

Katika Ibada hii, Kardinali Parolin atabainisha tunu msingi za maisha ya kiroho na kiutu zilizompelekea kujisadaka kwa ajili ya maskini na wote waliokuwa wanasukumizwa pembezoni mwa jamii ya wakati wake. NI Mama aliyekuwa na huruma na upendo wa pekee kwa wagonjwa, ndiyo maana Kardinali Parolin atakutana na Maaskofu wa Parague Hospitalini hapo. Jumapili tarehe 16 Novemba, 2014, Kardinali Pietro Parolin ataadhimisha Ibada ya Misa Takatifu katika Parokia ya Mtakatifu Agnese.







All the contents on this site are copyrighted ©.