Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania aliyefanyiwa operesheni ya tezi dume huko Baltimore,
Maryland, Marekani mwishoni mwa juma, anaendelea vyema na tayari ameanza kufanya mazoezi
kadiri ya taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu.
Rais
Kikwete anawashukuru watanzania na watu wote wenye mapenzi mema wanaoendelea kusali
na kumwombea dua jema ili aweze kupona hatimaye, kurudi Tanzania kuendelea na shughuli
za ujenzi wa taifa. Taarifa inawaomba wananchi kuendelea kusali kwa ajili ya Rais
Jakaya Kikwete.