2014-11-11 07:34:33

Zaidi ya wanafunzi 48 wameuwawa kikatili nchini Nigeria


Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu uliopita alitangaza hali ya hatari kwa majimbo yaliyoko kaskazini mwa Nigeria, ili kupambana na vitendo vya kigaidi vinavyofanywa na kikundi cha kigaidi cha Boko Haram, lakini hadi sasa watu wanaendelea kuuwawa kinyama na kutekwa na Boko Haram.

Siku ya Jumatatu, tarehe 10 Novemba 2014 zaidi ya wanafunzi 48 kutoka Chuo cha Ufundi, kilichoko Kaskazini mwa Nigeria wameuwawa kikatili baada ya kulipukiwa na bomu la kujitoa mhanga, wakati wanafunzi hao walipokuwa wamejipanga kwenye mstari, tayari kuanza kuingia madarasani. Mji wa Potiskum ni maarufu sana kwa masuala ya uchumi na biashara, Kaskazini mwa Nigeria, eneo ambalo limekuwa likiandamwa kwa mashambulizi ya kigaidi yanayofanywa na kikundi cha Boko Haram.







All the contents on this site are copyrighted ©.