2014-11-11 15:52:32

Ujumbe wa Papa kwa Mkutano wa 67 wa CEI.


Baraza la Maaskofu la Italia, CEI, Jumatatu lilianza Mkutano wake Mkuu wa 67 katika kituo cha kiroho cha Assisi ambao unaendelea hadi Alhamisi Novemba 13.

Ujumbe wa Papa Francisco kwa ajili ya Mkutano huu , ameonyesha ukaribu wake wa kiroho kwao na kwa kanisa, akiwaombea Roho wa Mungu awajalie kama Wachungaji. Roho huyo , aweze kulisha ubunifu na tumaini la Mkutano huo , ambao unalenga hasa katika kutazama kwa kina maisha, malezi na utume wa kudumu wa Padre.

Aidha Papa ameutumia mkutano huo kuwashukuru Maaskofu kwa dhati kwa utume wao mbalimbali wanaofanikisha kupitia kutembelea Parokia , mihadhara, utoaji wa elimu kwa vijana, na familia, wagonjwa majumbani na hospitalini, na kuwajali waliopungukiwa na watu maskini, bila ubaguzi. Amewasifu kwa kufanya hivyo kwa uhuru wao kamili binafsi na bila malalamiko, wakitembea pamoja katika upendo na wito wa Injili , na katika furaha iliyo ya kweli zaidi na haki katika maisha ya udugu.

Ujumbe wa Papa unaendelea kueleza , kwa mkutano huu kufanyika Assisi, kunamfanya apate hisia kali kwamba, ni Upendo Mkuu wa Mtakatifu Francisco, uliolilishwa na Utakatifu wa hirakia ya utawala wa Mama Kanisa, na kwa ajili ya makuhani. Na kisha Papa alikumbusha wajibu muhimu wa Maaskofu, katika kuimarisha watumishi wa Kanisa, linaloundwa na watu wa Mungu, ambao kwa ushuhuda wao makuhani, wametoa mchango mkubwa katika maisha yaliyowekwa wakfu. Na kwamba wameweza kujionea mng’ao wa maisha ya waumini wakati wa mihadhara, majadiliano na watoto, kusaidia familia, kutembelea wagonjwa nyumbani na hospitalini, kutunza maskini.
Ujumbe wa Papa unaendelea kusema Makuhani Watakatifu ni wale walio samehewa dhambi na kuwa vyombo vya msamaha, wenye kujiweka daima katika mikono ya Yule ambaye ahadi yake haipungui na ufahamu wao huongezwa na upendo kichungaji kwa watu waliokabidhiwa.

Ndiyo maana, anaandika Papa - bado ni muda unaofaa kwa makuhani, kwa wakati huu, kujenga madaraja ya kukutana kati ya Mungu na dunia. Kwa ajili hiyo, Papa Francisco pia alisisitiza kwamba, haifai seminari, kuharakisha kutoa daraja la ukuhani kwa wale wanaowania Maisha yaliyowekwa wakfu. Ni lazima kupima kwa kina, ukweli wa nia na malengo ya wale wanaotaka kuingia katika maisha yaliyowekwa wakfu ,kuyatolea maisha yao kwa ukarimu, katika hija ya maisha ya kumtumikia Yesu Kristo. Mafunzo, kwa hiyo, ni lazima kuambatana na uzoefu wa uanafunzi wa kudumu, ambao hauna mwisho, kwa sababu makuhani kamwe hawakomi kuwa wanafunzi wa Yesu. Kwa Papa Francisco, amesema, mafunzo ya awali na yale ya kudumu yasiyokuwa na mwisho huwa na sehemu mbili za ukweli wa umoja unaoendelea katika njia kudumu ya kuwa Padre mwanafunzi , katika upendo wa Mola wake.

Na hivyo Papa anaendelea inakuwa ni tumaini katika kuiishi siku, inayoongoza katika njia mpya ya kujifunza, majiundo ya kudumu na uwezo wa kuunganisha mitazamo mipana ya kiroho na ile ya kitamaduni, na mwelekeo wa Jumuiya ya kichungaji, kama nguzo za maisha thabiti ya kiinjili, yanayohitaji kudumishwa na nidhamu ya maombi ya kila siku, huduma binafsi, unyenyekevu na ushuhuda wa kinabii; Maisha yaliyohuishwa upya katika kanisa kwa uaminifu wa kuwekwa katika nafasi ya kwanza, miongoni mwa waamini.








All the contents on this site are copyrighted ©.