2014-11-11 16:02:41

Papa akutana na Maaskofu wa Afrika Magharibi


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu, aliwapokea Maaskofu wanaounda Baraza la Maaskofu la mataifa kadhaa ya Afrika Magharibi, Senegal, Mauritania, Cape Verde na Guinea Bissau, ambao wako katika ziara yao ya kila baada ya miaka mitano,” ad limina Visit”.
Akizungumza nao, Papa alionyesha kutambua kwamba, katika nchi hizi za Afrika Magharibi, ambako mara nyingi Wakristo ni sehemu ndogo, bado hujitoa kwa ukarimu zaidi kwa ushujaa wa kushuhudia Injili. Na hivyo inahitaji Maaskofu kufanya kazi ya ziada kupitia majadiliano ya kujenga ushirikiano thabiti zaidi na Waislamu. Na kwamba, kukutana nao , imekuwa ni nafasi kwake yeye na pia kwa Maaskofu hao kuimarisha kiungo cha upendo kati yao na hasa kwa makanisa yao na kanisa la Roma.

Hotuba ya Papa , ilifanya rejea kutoka katika waraka wake wa Injili ya Furaha, akiwahimiza Maaskofu kuendelea kuhudumu utume wa Kanisa kama wainjilishaji waliojawa na Roho wa kuinjilisha kwa sababu Roho Mtakatifu pia ataendelea kuwaunganisha na kuwajaza na ujasiri wa kutangaza kwa ushupavu Injili katika maisha yao ya kila siku na kila mahali. Papa alieleza huku akionyesha kutambua mazingira magumu yanayokabili mabaraza yao katika maana ya lugha ya kutumia, utamaduni na mapito ya kihistoria katika nchi zao.
Papa alizungumzia haja ya kwa walei ,katika majimbo yao , kupokea mafundisho thabiti na roho ya majiundo kwa ajili ya kutoa ushuhuda wa kuonekana kwa Kristo, katika mazingira ya jumuiya zao. Injili ni lazima iingizwe katika maisha ya kijamii kwa misingi ya kiinjili. Imani isipuuzwe katika maisha ya kijamii.
Aliendelea kuwahimiza kwamba, zaidi ya yote ya mizizi ya imani katika maisha ya watu, hasa katika kukabiliana na vitisho dhidi ya mapendekezo ya kidini, na hasa katika kuzingatia maadili. Aliwataka Maaskofu wasiongope kukemea mambo yanayoweza kuhatarisha maisha bora kwa jamii za Kiafrika, ambayo kwa sasa inakabiliwa kutokana na uzushi wa malimwengu.

Papa Francisco aliendelea kuelekeza mawazo yake kwa familia, hasa katika mwanga wa majadiliano yaliyofanyika katika Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya familia. Papa anasisitiza kuwa "familia ni kiini ya msingi kwa jamii na Kanisa. Familia ni mahali ambapo, misingi ya imani, kanuni ya msingi ya maisha ya jumuiya hufundishwa. Na ni ndani ya familia ambamo mara nyingi huzaliwa ya miito ya kikuhani na Utawa, kwa ajili ya katika Kanisa. Aidha Papa aliwataka Maaskofu waendelee kwa ushupavu zaidi na mjadala wa kujenga na mahusiano bora na Waislamu, mazungumzo katika haja ya kuishi kwa amani na mshikamano. Wakati huo huo, alionya, Kanisa lazima kushuhudia upendo wa Mungu kwa watu wote, bila "tofauti za kidini katika hatua ya kijamii."

Francisco, alisifu juhudi zinazo fanywa na Kanisa katika kudumisha amani katika mataifa mengi ya Afrika Magharibi, akionyesha kutambua mchango wa Kanisa, katika maendeleo ya binadamu, afya na elimu. "Baadhi ya Makanisa yako licha ya uchanga wake na umaskini wake, bado huwa na ujasiri katika mawasiliano na ukarimu wa imani.









All the contents on this site are copyrighted ©.