Jengeni utamaduni wa watu kukutana na kushikamana ili kudumisha amani!
Jumuiya ya Kimataifa inafanya kumbu kumbu ya miaka 25 tangu kuanguka kwa Ukuta wa
Berlin, kielelezo cha siasa za chuki na ubaguzi, mwaliko kwa watu wa kizazi hiki kujitahidi
kushiriki katika mchakato wa ujenzi wa madaraja yanayowaunganisha watu badala ya kuendeleza
kuta zinazowatenga watu!
Baba Mtakatifu Francisko, wakati wa Sala ya Malaika
wa Bwana, Jumapili tarehe 9 Novemba 2014 kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu
Petro, aliwaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kusali na kumwomba Mwenyezi
Mungu ili aweze kuwasaidia kujenga utamaduni wa watu kukutana.
Katika ujumbe
wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii na watu wote wenye mapenzi mema, Baba Mtakatifu
anakazia kwa namna ya pekee, utamaduni wa watu kukutana, kushikamana na ujenzi wa
amani.