2014-11-10 12:22:45

Papa:Mkristo usiwe chanzo cha kashfa ila msamaha


Kamwe Mkristo usiwe chanzo cha kashfa, lakini daima mtu wa kusamehe, na mtu wa imani. Kila Mkristo, katika kila njia ya wito wake katika utendaji wa maisha ya kila siku, anapaswa kutanguliza kusamehe na kamwe si kusababisha kashfa, kwa sababu "kashfa huharibu imani." Papa Francisko ameonya wakati akiongoza Ibada ya Misa mapema Jumatatu hii , katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta ndani Vatican.

Papa alieleza na kurejea maneno ya Yesu kwa wanafunzi wake ambamo alionye heri kujifungia jiwe shingoni na kujitupa bahari kuliko kuwakosesha wadogo hawa. Homilia ya Papa Francisco ilienga katika somo la Injili ya Luka, ambamo kuna maneno matatu muhimu: dhambi, msamaha na imani.
Ole wao hao wanaowakosesha wengine anaonya Kristo. Na pia Mtume Paulo alivyomwandikia Tito, anatoa maelekezo sahihi juu ya jinsi ya kutembea katika njia ya maisha ya kikuhani. Si kuwa mtu wa vurugu, lakini mtu wa kiasi kwa kila jambo, na wabwabwajikaji na mtu wa kuzua kashfa. Na hili si kwa makuhani tu lakini kwa Wakristo wote.
Aliendelea kutaja mifano ya kukashfu imani, akisema kama yule mtu anaye jiita Mkristo, katika kusema na katika kukiri njia ya maisha, lakini ndani mwake haamini chochote na maisha yake yako nje ya Ukristo. Hii inakuwa ni kashfa kwa sababu hakuna kinachoshuhudia imani anayokiri.
Pia mfano wa Mkristo au Wakristo, ambao huenda kanisani, kwenda kusali, lakini hawayaishi maisha ya Kristo, bali huyagandamiza, huko pia ni kuikashfu imani. Na pia kuwa wengine ambao husema, mimi siendi Kanisani, wanaume au wanawake wanao heri kubaki nyumbani kuwa kama hao wanaokwenda kanisa lakini kisha wakitenda ovyo kwa hili au lile, kama vile si wabatizwa. Hii ni kashfa kubwa inayo haribu imani! Na ndiyo maana Yesu alisema kwa nguvu: jihadharini! Na hata leo hii ni vyema kurudia maneno hayo, Jihadharini, kwa kuwa sote ni dhaifu katika kusababisha kashfa.

Na kumbe sote tunapaswa kujua jinsi ya kusamehe mapungufu ya wenzetu na kusonga mbele pamoja ktiakmwendo wa imani. Ni kusamehe daima, Papa alisisitiza, kama Yesu alivyosema, zaidi ya mara saba kwa siku wakati tunadhulumiwa.Hapo Kristo alionyesha maana na umuhimu wa kusamehe, hivyo Mkristo asiyeweza kusamehe , huyo si Mkristo.


Kusamehe ni Sala ya Bwana, aliyofundisha na Yesu mwenyewe. Papa alionya, si rahisi sisi kuelewa katika mantiki ya kibinadamu. Mantiki ya binadamu hutoongoza katika nia za kutotaka kusamehe, bali kujenga kisasi; chuki na mgawanyiko. Papa alieleza na kuhoji ni familia ngapi zimevunjika, au watoto kutengwa na wazazi wao, waume na wake, kwa sababu za kutosamehe?.... Ni muhimu kufikiria hili kwamba, kusamehe si kupoteza haki, lakini kuna maana ya kukubali kwamba Mungu pia ananisamehe mimi kwa makosa yangu. Hivyo sisi sote yatupaswa kulielewa hili. Papa Francisco alieleza na kuongeza bila shaka sasa tunaelewa kwa nini wanafunzi wa Yesu waliposikia maneno haya ya kusamehe kutoka kwa Bwana, waliongeza imani yao.

Daima ni Kukumbuka, haiwezekani kujiepusha na kashfa na kuwa mtu wa kusamehe bila kuwa mtu wa imani. Ni tu kwa mwanga wa imani, ile imani tumepokea kutoka kwa Baba mwenye huruma, Mwana ambaye alitoa maisha yake kwa ajili yetu, Roho wake anayeishi ndani mwetu , hutusaidia kukua katika imani, ndani ya imani ya Kanisa, imani ya watu wa Mungu, waliopokea ubatizo na kutakatifushwa. Na hii ni zawadi. Imani ni zawadi inayotoka kwa Mungu, aliyo wamwangia mitume wa Yesu , walioomba:“tuongezee imani” .








All the contents on this site are copyrighted ©.