Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 7 Novemba 2014, amekutana na kuzungumza kwa
faragha na Kardinali Angelo Amato, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa linalowatangaza
waamini kuwa Wenyeheri na Watakatifu na kumruhusu kuchapisha hati zinazowahusu Watumishi
wa Mungu wanane, ambao sasa wameanza mchakato, ili waweze kutangazwa kuwa ni Wenyeheri
kadiri ya mpango wa Mama Kanisa.
Kati ya Watumishi wa Mungu wapya, yumo mtoto
mwenye umri wa miaka kumi na miwili Silvio Dissegna; Mwalimu wa vijana Padre Raismondo
Calgano. Wengine ni Francesco Massiano Valdes Subercaseaux; Ildebrand Gregori; Giovanni
Sullivan, Pelagio Sauter, Giovanna Mance, mwamini mlei; Marta Luigia Robin, mwamini
mlei na mwanzilishi wa Chama cha Foyer de Charitè, Ufaransa.