2014-11-08 15:01:25

Papa akutana na wanachama wa Scouts .


Baba Mtakatifu Jumamosi hii amekutana na Maskauti Katoliki wa Italia , ambao kwa sasa ni watu wazima, waliombelea kama sehemu ya maadhimisho ya Sikukuu yao ya kutimia miaka 60 tangu kuanzishwa chama cha Maskauti Katoliki cha Italia.
Katika hotuba yake kwa Maskauti hao, Papa alitoa shukurani zake za dhati kwa kazi yao ya miaka sitini ambamo wameweza kuonyesha ushuhuda wa kitume katika Kanisa na katika jamii, maadili ya uaminifu, udugu na upendo kwa Mungu na jirani. Papa aliendelea kuwataka waendelee kutembea katika njia hiyo, na kwa matumaini ya baadaye.
Jumla ya wanachama 7000, Wakiwakilisha Maskauti watu wazima, nchini Italia, walipokelewa na Papa katika Ukumbi wa Paulo VI. Chama hicho kilianzishwa mwaka 1954 na Mario Mazza. Shamra shamra za mkusanyiko huo zilipambwa kwa nyimbo na shuhuda. Ilikuwa ni kanisa linalo toka na kwenda nje kuhudumia kama Papa Francisco anavyopenda kanisa liwe.
Rais na Katibu wa Kitaifa kwa chama hiki kinachojukana kama Masci, alisema wanapenda daima kuwa mashahidi wa ushupavu, wasiokuwa na woga wa kuingia ndani kwa ajili ya kuifikisha imani . Kwa ajili hiyo, Papa aliwashukuru wote na kuwaomba waendelee na wito huo, katika safari yao, wakingoza katika njia ya kweli kwa familia, licha mahangaiko ya kieleo, daima washikilie katika kuitafuta njia ya haki, wakitembea kwa utulivu daima katika kuongoza njia!

Papa katika hotuba yake ametaja mazingira matatu muhimu , nayo ni familia, kama kiini cha jamii, jamii ya upendo na maisha bora, katika jinsi ya kuhusiana na wengine na dunia. Na kwamba inatakiwa kuzingatia hili tangu hatua zake za kwanza za maisha.
Na kwa vyama kama hiki, ambavyo hujifunza njia za maisha na juu ya uchaguzi wa elimu, ni muhimu kuthibitisha kwamba, elimu ndani ya familia ni kipaumbele cha kwanza katika uchaguzi. Na hivyo kwa Wazazi Wakristo, utume wa elimu uweze kuchipuka kutoka katika sakramenti ya ndoa, ambamo ndani yake mna kazi ya kuwalea watoto kama huduma ya kweli kwa Kanisa.

Ni kutengeneza njia kwa mjibu wa maisha ya kiskauti. Kama wanafunzi wa Kristo, Papa anasema, tuna kila sababu ya kulinda na kutetea zawadi tuliyopewa na Muumba, "tunatambua alama yake kwa wenzetu walioumbwa kwa mfano na sura yake.

Papa aliendelea kueleza kwamba , tunaishi katika mashinikizo mengi ya mazingira na asili,lakini kama maskauti wanavyotenda , haionyeshi tu kujiheshimu wao wenyewe lakini pia ahadi ya kuchangia vyema na kuondoa yale yanayoichafua jamii inayokuwa na mwelekeo wakutaka kuyaangamiza yaliyo mema kwa jamii , na pia katika kujitolea kwao katika mahitaji ya kijamii.

Papa alikamilisha hotuba yake kwa Maskauti na wito wa kuwa chachu ya kwa ajili ya utambuzi wa mema ya kawaida na kuonyesha kama dira, "moyo ulioelekezwa kukutana na hisia ya Mungu. amesema , katika utata wa kitamaduni kwa jamii ya leo, kushuhudia kwa unyenyekevu, kwa ajili ya kuonyesha unyenyekevu upendo wa Yesu kwa watu wote, na uaminifu wa wakristo katika huduma zao, inaweza kuwa ni chachu kwa wale waliopoteza upeo wa kuona uwepo wa Mungu. Ni muhimu kuwa dira ya kweli ya maisha kwa wake na waume, katika kuuleta karibu moyo, moyo unaokuwa na mwelekeo mpya katika hisia za kukutana na Mungu.







All the contents on this site are copyrighted ©.