Askofu Christopher Kakooza ateuliwa kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki Lugazi, Uganda
Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi la Askofu Matthias Ssekamanya wa Jimbo Katoliki
Lugazi kung'atuka kutoka madarakani kadiri ya sheria za Kanisa namba 401, Ibara ya
1. Wakati huo huo, Baba Mtakatifu amemteua Askofu msaidizi Christopher Kakooza kutoka
Jimbo kuu la Kampala, Uganda, kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Lugazi, Uganda.
Itakumbukwa
kwamba, Askofu Christopher Kakooza alizaliwa kunako tarehe 15 Novemba 1952 hujko Lusaze,
Uganda. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 3
Juni 1983. Tarehe 2 Januari 1999, akateuliwa na Papa Yohane Paulo II kuwa Askofu msaidizi
wa Jimbo kuu la Kampala, Uganda na kuwekwa wakfu hapo tarehe 17 Aprili 1999.