Bwana Filipe Yacinto Nyussi aliyekuwa anapeperusha bendera ya FRELIMO katika uchaguzi
mkuu uliofanyika hivi karibuni nchini Msumbiji, ameibuka kidedea kwa kupata asilimia
57.3% ya kura zote halali zilizopigwa wakati wa uchaguzi na hivyo kufanikiwa kuwa
ni Rais wa Msumbiji.
Tume ya uchaguzi nchini Msumbiji tarehe 30 Oktoba 2014
imemtangaza Bwana Nyussi kuwa Rais Mpya wa Msumbiji. Chama cha FRELIMO kimefanikiwa
kujinyakulia viti 144 vya ubunge kati ya viti 250 vya bunge zima. RENAMO limefanikiwa
kujinyakulia viti 89 vya Ubunge na Bwana Alfonso Dhlakama aliyekuwa kwenye kinyang'anyiro
cha urasi amejipatia asilimia 36.6% ya kura zote halali zilizopigwa. Chama cha MDM
imefanikiwa kupata viti 17. Bwana David Simago aliyekuwa anawania Urais amepata kura
chini ya asilimia 6% ya kura zote halali zilizopigwa.