Wachezaji wa Bayen Munich wakutana na Papa baada ya kuichabanga Roma kwa mabao 7-1
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 22 Oktoba 2014 kabla ya Katekesi yake kwa
wageni na mahujaji kutoka sehemu mbali mbali za dunia, alikutana na kuzungumza na
wachezaji wa timu ya mpira F.C. Bayen Munich kutoka Ujerumani baada ya mashindano
kati yake na timu ya A.S. Roma iliyochabangwa magoli 7- 1, jambo ambalo liliwasikitisha
sana mashabiki wa timu ya Roma.
Viongozi wa Timu ya Bayen Munich walimzawadia
Baba Mtakatifu mpira ambao ulikuwa una majina ya wachezaji wote wa timu ya Bayen Munich
pamoja na kumpatia Jezi maalum iliyoandikwa kwa lugha ya kijerumani, "Franziskus".
Timu hii ya Mpira itamzawaidia Baba Mtakatifu Francisko kiasi cha Euro Millioni moja
katika mashindano mbali mbali ya kirafiki yatakayofanywa na Timu hii katika kipindi
cha mwaka mzima.
Baba Mtakatifu ataitumia fedha hii kwa ajili ya kuwasaidia
maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.