Mababa wa Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia iliyohitimishwa hivi karibuni
walipata nafasi ya kusali, kutafakari na kushirikishana kwa kina na mapana tunu msingi
za maisha ya ndoa na familia, tayari kutweka hadi kilindini, ili kuwatangazia Watu
wa Mataifa, Injili ya Familia. Hii ni kazi kubwa iliyofanywa na Mababa wa Sinodi kwa
ushiriki wa Baba Mtakatifu Francisko, kama Khalifa wa Mtakatifu Petro ambaye ni kielelezo
cha mshikamano na umoja wa Kanisa la Kristo!
Baba Mtakatifu Francisko katika
ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema kwamba, familia ni mahali
ambapo mwanadamu anapata majiundo makini. Kila familia ni tofali katika mchakato wa
ujenzi wa jamii!