2014-10-13 10:13:33

Waguswa na mahangaiko ya wanawake na wasichana huko Mashariki ya Kati!


Mashirika ya Wanawake Wakristo na Waislam kutoka nchini Australia, kwa pamoja yameguswa na mahangaiko pamoja na mateso ya wanawake na wasichana walioko nchini Syria, Iraq na baadhi ya nchi za Kiafrika. Vyama hivi vinalaani vitendo vinavyopelekea ubaguzi wa kidini unaofanywa dhidi ya waamini wa dini mbali mbali duniani.

Kwa namna ya pekee, wanasikitishwa na chuki na uhasama wa kidini wanaofanyiwa Wakristo huko Mashariki ya Kati. Mashirika haya katika tamko lao, wanasema wameguswa na mahangaiko ya wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi na kwamba, Jumuiya ya Kimataifa inaweza kupata mafanikio ikiwa kama watu wataonesha moyo wa toba na huruma kwa kujikita katika hali ya kuvumiliana na kusaidiana, huku wakitambua kwamba, tofauti zao za kidini ni utajiri mkubwa na mpango wa Mungu kwa binadamu.

Mashirika haya yanawataka viongozi wa kimataifa kuhakikisha kwamba, wanasaidia kulinda na kudumisha haki msingi za binadamu sanjari na uhuru wa kuabudu.







All the contents on this site are copyrighted ©.