Papa: Biblia isomwe kila siku na zaidi Jumapili ndani ya familia
Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili wakti wa sala ya malaika wa Bwana alikumbusha juu
ya ufunguzi wa Sinodi maalumu ya Maaskofu , Kwamba, Maaskofu wanaotoka pande zote
za dunia, kwa muda wa wiki mbili watajadili changamoto za kichungaji kwa familia
katika mtazamo wa Kazi za kichungaji na uinjilishaji.
Papa aliangalisha pia
katika liturjia ya Jumapili, akisema ilionyesha picha ya shamba la mizabibu, kama
ishara ya watu, wanaochaguliwa kulihudumia Kanisa, kama shamba la mizabibu lenye
kuhitaji watu kulitunza kwa upendo, subira na uaminifu.
Na ndivyo hivyo
Mungu anavyofanya kwa watu wake walioitwa kuwa wachungaji. Kutunza familia ya watu
wa Mungu, ni kufanya kazi katika shamba la Bwana ili shamba hili lipate kutoa matunda
ya ufalme wa Mungu (Mt 21,33-43), Lakini ili familia ipate kutembea vema , kwa imani
na matumaini, inapaswa kulishwa Neno la Mungu, na ndiyo maana ni furaha kuona ndugu
wa familia wa Mtakatifu Paulo "Paulini", wametaka kugawa Biblia katika Uwanja wa
Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro na sehemu mbalimbali
Papa aliongeza kwamba,
wanafanya ishara hiyo kwa ajili ya kuadhimisha siku ya mwanzilishi wao wa shirika
Mwenye Heri Giacomo Alberione, mtume shupavu katika mawasiliano.
Kwa namana
hiyo wakati Sinodi imefunguliwa kwa ajili ya familia, kwa msaada wa Wapaulini, Papa
anasema ina maana “Kila familia iwe na Biblia”Lakini isiwekwe pemebeni mwa kabati
tu, bali iwe mkononi daima, isomwe kila siku, iwe na kibinafsi au kwa pamoja mke
na mme,au kama familia wazazi na watoto, wakati wa usiku, na zaidi siku ya Jumapili.
Ni kwa njia hiyo familia itakua, na kutembea na mwanga na nguvu ya Neno la Mungu.
Na mwisho, Papa aliwaalika wote kusindikiza kwa sala, kazi ya Sinodi, kwa maombezi
ya Bikira Maria. Aliwakumbusha kuungana kiroho katika maombezi kwenye Madhabahu ya
Pompei kama utamaduni wa sala kwa mama Maria wa Rosari, azijalie amani familia na
Ulimwengu mzima.
Vile vile baada ya sala ya Malaika wa Bwana, Papa kwa kifupi
alizungumzia kutangazwa kwa Mwenye Heri Sr Maria Teresa Demjanovich wa Marekani
wa shirika la Upendo la Mtakatifu Elizabeth, siku ya Jumamosi Oktoba 4, akisema ni
jambo la kumshukuru Mungu kwa ajili ya neema ya Mungu kwa Mtumishi wa Kristo aliyeishi
kwa kina maisha ya kiroho.
Aliwasalimia mahujaji wote waliotoka nchini italia
na pande zote za Dunia, na hasa wanafunzi kutoka nchini Austraila, Ujermani, Jordan,Chama
cha Mtakatifu Giovanna de Mathsa, na waamini kutoka Parokia za Mtakatifu Paulo uko
Bergamo italia. Mahujaji waliofikia kwa baiskeli kutoka Milan akimkumbuka Mtakatifu
Gianna Beretta Molla Matakatifu na mama wa familia na mtoa ushuhuda wa Injili ya Maisha,
na waliwatia moyo kuendeleza na ushuhuda wao kwa mshikamano kwa watu walio wadhaifu.