2014-10-01 08:50:57

Epukeni malalamiko kama vile mko katika ukumbi wa sanaa, kwani wapo wanaoteseka kweli


(Vatican Radio) Kulalamika wakati wa kipindi cha giza ni sala lakini angalieni kuepuka malalamiko kama wale walioko kwenye ukumbi wa sanaa, kwa ni wapo wenye shida za kweli wanaostahili kulalamika kama vile wale wanaoishi katika majanga makubwa ya mateso mfano Wakristo wenzetu waliofukuzwa katika makazi yao kwa sababu ya imani yao.

Ni homilia ya Papa Fransisko Jumanne 30 Septemba wakati wa Ibada ya Misa, ndani ya Kanisa dogo la Mtakatifu Marta Vatican. Akichambua somo la kwanza kuhusu historia ya Ayubu anayelaani siku ya kuzaliwa kwake , Papa alisema kwamba, aliwekwa katika majaribu, kwani alipoteza familia yake yote, alipoteza utajiri wake wote , akapoteza afya ya mwili wake, na ukawa ni vidonda tupu vya kutia kinyaa. Papa aliongeza, wakati huo Ayubu alipoteza subira, na kusema maneno hayo ambayo siyo mazuri. Lakini yeye alizoea kusema ukweli , na ndiyo maana muda huo alikuwa akisema ukweli, Papa aliuliza swali je huyo mtu alikufuru? Mwanadamu huyo aliyechwa peke yake, je alikufuru?

Je Yesu alipolalamika kwamba Baba kwanini umeniacha je alikurufu, ni fumbo hilo. Papa alisema kwamba amesikia mara nyingi watu wanaishi katika hali ngumu , na ya uchungu,na wamepoteza mengi na wanajisikia upweke, wameachwa , na kulalamika wakijiuliza kwa swali hilo kwanini?, wanamkasirikia Mungu… Lakini Papa aliwataka waaamini waendelee kusali hivyo, kwasababu swali hilo ni sala, kwa maana ilikuwa vilevile ni sala hata Yesu alipomweleza Baba yake kwamba mbona umeniacha.

Sala ya Ayubu inajionyesha kwamba kusali ni kuwa mkweli mbele ya Mungu, na Ayubu ilimpasa kusali hivyo kwa hali yake, maana sala ya kweli ni ile itokayo rohoni kutokana na hali unayoishi, ni sala wakati wa kipindi kigumu na cha shida, ni wakati wa maisha kama vile hakuna matumaini, ni wakti si rahisi kuona upeo.

Aliongeza kwamba watu wengi leo hii wako katika hali kama ya Ayubu, na ni watu wema kama Ayubu hawajui na hawajui kwa nini hali hiyo imewatokea. Ndugu zetu kaka na dada hawana matumaini , ukifikiria majanga na ghasia za wakristo wenzetu waliofukuzwa katika nyumba zao na kubaki bila kitu chochote ,nao wanajiuliza, Bwana mimi nilikuamini, kwani kukuamini wewe ni kulaamiwa Bwana?

Papa aliendelea kuwataka waamini wawafikirie wazee waliofukuzwa, wagonjwa, na watu wengi wenye upweke mahospitalini, na kwa watu hao aliwataka wakumbuke kwamba Kanisa linasali kwa ajili yao, na linateseka pamoja nao katika uchungu wa mateso yao.
.
Papa kisha aliwageukia na swali wale ambao hawana ugonjwa, njaa, shida ya mahitaji yoyote, wanapopata giza rohoni, je wanamwacha Mungu na kuacha kusali? Kwani alibainisha kwamba wapo watu kama hao wanasema , nimemkasirikia Mungu , siendi Misa tena je ni kwanini? Papa aliuza. Kwaajili ya kitu kidogo tu. Alitoa mfano mmoja kuhusu Mtakatifu Teresa wa mtoto Yesu mwishoni mwa maisha yake , alipata giza la namna hiyo rohoni akifikiria kuona mbingu ndani mwake, lakini aligundua kwamba alikuwa anajidanganya na ndoto zake.

Papa Francisco aliendelea kwamba mara nyingi tunajisikia katika hali hii na kuishi katika hali hiyo.Watu wengi wanajisikia kuishi kama vile hawafanyi lolote. Lakini Mtakatifu Teresa alikuwa akisali na kuomba nguvu ya kuendelea mbele katika giza hilo . Njia hiyo inaitwa subira . Kwani maisha yetu, maisha ya wengi ni rahisi kuishi katika hali ya kulalamilka kama ulalamikavyo umati wa watu waliokusanyika katika ukumbu wa michezo, wanapopatwa na matatizo kidogo.. Ni hali ya watu wengi ndugu zetu wanaoishi katika giza hata kupoteza matumaini. Wengi wanaishi katika kilindi cha kujisahu wenyewe. Pia Yesu alipitia katika njia hiyo , katika mlima wa mizeituni hadi njia ya msalaba na kusema Baba mbona umeniacha.

Papa Francesco alimalizia homilia yake akitoa maelekezo ya njia mbili za kufuata wakati wa kipindi cha giza kwamba, kwanza ni kujiandaa na kipindi cha giza litakalokuja, na pili kusali kama Kanisa linavyosali kwa ajili ya ndugu wanaoteseka kwenye bonde la machozi katika kipindi hiki cha mateso, na ukosefu wa matumaini . Hiyo ndiyo sala ya kanisa.








All the contents on this site are copyrighted ©.