Kardinali Pietro Parolini : Watu wote wabebe jukumu la kulinda mazingira.
(Vatican Radio) Katika Mkutano Mkuu wa 69 wa Umoja wa Mataifa unaondelea huko mjini
New York Marekani, Katibu wa Vatican Kardinali Pietro Parolini ametoa ujumbe wake
kama mwakilishi wa Papa katika Mkutano huo.
Amesema, ni bayana kwamba, mabadiliko
ya tabianchi hayaangalii tu sayansi, mazingira, siasa na uchumi , bali yanagusa masuala
yote hata maadili ya mwanadamu, kwa sababu jamii ndiyo inaathirika na hasa watu
masikini kati yetu. Vatican mara nyingi imesisitiza umuhimu wa uwajibikaji katika
utendaji ili kwamba kila mmoja aweze kubeba jukumu la kulinda na kuthamini viumbe
kwa ajili ya uzuri wa dunia kwa sasa na kwa vizazi vijavyo.
Vilevile alikumbusha
kwamba , Tangu mwanzo wa utume wake, Papa Francisko amekuwa akisisitiza suala la
kulinda mazingira yetu. Lakini bado kuna matumizi mabaya ya mazingira, badala ya
kutumika vema, yanachakazwa, kunyonywa na kusababisha madhara makubwa.
Utafiti
wa kisayansi unathibitisha kwamba tangu nusu ya miongo ilioyopita kumekuwa na ongezeko
la joto kupita kiasi. Ni tatizo kubwa na hasa kwa madhara ya sekta ya jamii inayo
ishi katika mazingira magumu na zaidi itakuwa pia kwa vizazi vijavyo. Tayari inadhihirika
gharama za uchumi, na tatizo ongezeko la hewa chafu ya ukaa angani ni matokeo ya
utendaji mbovu wa shughuli za binadamu.
Kardinali Parolini anabainisha, katika
kukabiliana na hatari za gharama hizi, ni busara kuchukua hatua za kuzuia , ambazo
zinahitaji uamuzi sahihi wa kutenda ukizingatia pia mazuri ya siku zijazo. Hili ni
hitaji na uwajibikaji mkubwa katika dhamira ya kisiasa na kiuchumi kwa Jumuiya ya
Kimataifa , ambayo pia Vatikan inatoa mchango wake ikiwa inatambua kwamba “zawadi
ya maarifa inasaidia kutoangukia katika dimbwi la mafanikio yasiyo jali uharibifu.
Kupambana na tatizo la ongezeko la joto duniani linahitaji umakini siyo
tu kuimarisha, au kukuza mchakato wa kisiasa katika ngazi ya kimataifa, lakini pia
ni kuwa waaminifu katika ahadi zetu zinazodai mabadiliko katika utendaji na kugundua
zaidi juu ya maadili msingi ambao familia na jamii nzima ya binadamu inaweza kujengwa
juu yake.
Vatican inalenga katika utendaji wenye uwajibikaji, na inatambua
kuwa Jumuiya ya kimataifa itaweza kuongozwa na utendaji adilifu, kwa mujibu wa kanuni
ya mshikamano na manufaa ya wote, katika utambuzi wa kuheshimu msingi ya haki kwa
kila binadamu. Huu ni wajibu kwa kila binadamu, unaotakiwa kutekelezwa kwa manufaa
ya wote, na kwa ajili ya kuboresha na kupatia sura mpya, mambo yote ya uchumi na
siasa.(Evangelii Gaudium, 203)