Ijumaa 19 Septemba katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta Vatican, Papa aliadhimisha
ibada ya Misa ambamo katika homilia yake,alilenga zaidi juu ya Neno la Mungu, kutoka
barua ya kwanza ya Mtakatifu Paulo kwa Wakorinto, ambamo Wakristo wanaonekana kuwa
na matatizio ya kuamini mabadiliko ya miili yao baada ya kifo.
Alisema kwamba
Mtume wa watu alikwenda kuwaeleza Wakristo Wakorinto, wale ambao waliamini kwamba
Kristu amefufuka, lakini walikosa mwanga zaidi kwamba hata na wao watafufuka, wao
walifikiri kwa namna nyingine, ya kwamba wafu wamekwisha hukumiwa.
Hata hivyo
siku ya kwanza ya Juma ya ufufuko wa Yesu , hata Mtakatifu Petro alikimbia kwenda
kaburini akifikiri kwamba mwili wa Bwana umeibiwa vilevile hata Maria wa Magdala.
Hawakukumbuka ufufuko wa kweli, walishindwa kuelewa njia ya kutoka katika kifo kuufikia
uzima ni kwa njia ya ufufuko.
Waliupokea ufufuko wa Yesu kwa sababu walimuona
Yesu. Papa aliongeza, hata hivyo ufufuko wa Wakristo haukuwa hivyo maana hata Mtakatifu
Paulo alipokwenda Atene na kuanza kuhubiri juu ya ufufuko wa Kristo watu walilamika,
mpaka wagiriki wenye hekima, na Wataalimungu waliogopa.
Ufufuko wa wakristo
ni kashfa, ni vigumu kuutambua, na ndiyo maana Paulo aliwaza hivi; “kama Kristo amefufuka
, inawezekanaje kati yenu kusema hakuna ufufuko katika wafu?”
Anabainisha
Papa, kuna ugumu wa kupokea mabadiliko, ugumu ambao kazi ya Roho Mtakatifu tuliyempokea
kwa njia ya ubatizo anao uwezo wa kubadili mpaka mwisho , hadi katika ufufuko.
Alitoa
mfano ,tunapoongea juu ya hilo , “tunasema mimi ninataka kwenda mbinguni, sitaki kwenda
ahera, natunasimama pale pale, hakuna anayesema ,mimi nitafufuka kama Yesu, hakuna,
kwa hiyo hata sisi ni vigumu kutambua jambo hilo.
Ni rahisi kwa wanaosadiki
kuwa ulimwengu wote kuna miungu wengi, sababu yake wanaamini kuwa kuna uwezekano wa
kubadilika, hata hivyo neno “kubadilika ”ni neno ambalo Mtakatifu Paulo alilitumia
ya kwamba tutabadilishwa. Miili yetu itabadilishwa, alitoa mfano wa jinsi watu hupatwa
na hofu wanapokuwa katika tiba ya kupasuliwa hospitalini, wana woga wa kutolewa kitu
fulani ndani ya mwili wao ,au kuwekewa kitu fulani… na hivyo kusababisha mabadiliko,
kwa kusema hivyo hata katika ufufuko wote tutabadilishwa.
Hali hiyo ndiyo inayotusubiri
siku zijazo , na ndiyo inayotufanya tuwe wagumu: ugumu hasa wa kubadilishwa miiili
yetu. Hata ugumu wa kuwa na uthibitisho wa Mkristo. Papa alitoa mfano mwingine
ya kwamba inawezekana hatuogopi ufunuo wa mabaya, au wale wanaompinga Kristu ambaye
atarudi tena, hatuogopi. Labda hatuna uoga wa sauti ya malaika, au sauti ya baragumu:kwakuwa
itakuwa ni ushindi wa Bwana.
Bali tunao woga wa ufufuko wafu. Wote tutabadilishwa,
na ndiyo utakuwa mwisho wa safari yetu ya ukristo, yaani ile ya kubadilishwa.
Lakini
kishawishi hiki cha kutokuamini ufufuo katika wafu, hata mwanzo kabisa wa Kanisa
ilikuwepo,hata Mtakatifu Paulo alipoongeea kwa watu Wathesalonike, katika barua yake
aliwatuliza na kuwatia moyo wawe na matumaini, maana mwisho tutakuwa naye.
Alimazia
kwa kusema kwamba uthibitisho wa Mkristo na njia yake , ni safari ambayo yupo Bwana
, kama wale mitume wawili waliotembea na Bwana na mwisho wakabaki naye jioni, tunaitwa
maisha yetu yote kuishi na Bwana , na mwisho tutakaposikia sauti ya malaika baada
ya mlio wa baragumu tutabaki naye.