(Vatican Radio) Ni mafundisho ya baba Matakatifu aliyoyatamka Alhamis 18 Septemba
katika mahubiri yake ndani ya kanisa dogo la Mtakatifu Marta Vatican. Papa alisema
Liturgia ya neno,leo inatufikisha katika tukio la mwanamke anaye muosha Yesu miguu
yake kwa machozi , na kumkausha kwa nywele zake, na kumpaka manukato.
Yesu
alikaribishwa kwenye nyumba ya mfarisayo mmoja, mwenye ujuzi na hata elimu, ambaye
alitaka kumsikiliza. Mafunzo hayo ilikuwa ni kutaka kujua zaidi, japokuwa anamhukumu
rohoni mwake yule mwenye dhambi, na kuhukumu pia Yesu mwenyewe akisema “kama angekuwa
ni nabii angejua ni nani mwanamke anayemgusa”
Papa aliongeza,Mfarisayo hakuwa
mbaya , bali hakufahamu kitendo kile alichotenda mwanamke. Alishindwa kuelewa ishara
msingi za watu, labda mtu huyo alikuwa amesahau namna gani wanavyo bembeleza watoto
, au kumfariji mzee.
Katika mafunzo yake, katika fikira zake, na katika maisha
ya utawala wake, labda alikuwa ni mshauri wa wafarisayo, alikuwa amesahabu ishara
msingi za maisha, ambazo kila mmoja wetu mara anapozaliwa alizipokea kutoka kwa wazazi
wake.
Yesu alimkaripia mfarisayo, aliongeza Papa, lakini kwa unyenyekevu,
huruma, subira, na upendo wake wa kutaka kuwaokoa wote, unamfanya Yesu awaelezee juu
ya ishara ya mwanamke kufanya kitendo hicho ya kwamba; hakumfanyia yeye.
Lakini pamoja na wengi kutoa kashifa na masengenyo kwa mwanamke huyo, wanasikia “dhambi
zako zimeondolewa, nenda kwa amani , imani yako imekuokoa” Neno Wokovu, Papa alisema,
imani yako imekuokoa, ni neno alilomweleza mwanamke mwenye dhambi, ni kwa sababu
alijutia dhambi zake, aliungama dhambi zake, na kusema yeye ni mwenye dhambi. Hakuwaeleza
wale ambao hawakuwa wabaya, wao waliamini hawana dhambi, wenye dhambi walikuwa ni
wengine, watoza ushuru na makahaba hawa ndiyo walikuwa wanahesabiwa wenye dhambi. Lakini
Yesu alisema umeokolewa wewe,ni maneno anayoyatoa kwa yule tu anayejua kufungua moyo
wake na kijitambua mwenye dhambi. Wokovu wa roho ni kwa wale tu wanaojua kujifunua
kweli na kutambua dhambi zao. Watu wenye dhambi wanayo nafasi mwafaka ya kukutana
na Yesu alibainisha Papa na kutoa mfano, katika jambo hili unaweza kufikiri ni uzushi
lakini hata Mtakatifu Paulo anajivunia kwa mambo mawili ya dhambi zake na ya Kristo
mfufuka aliye mwokoa, alidhihilisha Papa. Kwa namna hiyo kujitambua dhambi zetu
wenyewe, kutambua udhaifu wetu, ni kujiambua sisi wenyewe, kutambua kile tulicho
na uwezo nacho. pia kile tusichojua kufanya, ni dhahiri kuwa mlango unafungua njia
katika mbeleko ya Yesu, msamaha wa Yesu, na Neno la Yesu asemaye “Nenda kwa amani,
imani yako imekuokoa, kwakuwa umekuwa na ujasiri wa kufungua moyo wako kwa yule tu
ambaye anaweza kukuokoa. Yesu aliwambia wanafiki, makahaba na watoza ushuru watawatangulia
mbele katika ufalme wa mbingu…”Ni neno lenye uzito” alimalizia Papa, kwani wengi wanaojisikia
wadhambi, wanafungua mioyo yao katika sakramenti ya kitubio, kuungama dhambi na kukutana
na Yesu ambaye amemwaga damu kwa ajili ya wote.