Katibu kwa Mahusiano na Nchi zingine Vatican,Askofu Mkuu Domenique Mamberti, anatembelea
Georgia. Ziara aliyoianza siku ya Jumamosi na anakamilika Jumanne hii, Septemba 16,
2014.
Tarifa inaleza Jumatatu, Septemba 15 alikutana na Waziri Maria Panjikidze
wa Mambo ya Nchi za Nje Georgia, ambamo walijadili wigo mpana wa mahusiano baina
ya Vatican na Georgia, nchi na kusisitiza umuhimu wa ziara hii katika suala la Kuimarisha
uhusiano wa kirafiki kati ya mbili mataifa.
Na hivyo pande zote zilisisitiza
umuhimu wa ushirikiano wa karibu katika nyanja ya kitamaduni, kielimu na kibinadamu.
Askofu Mkuu Dominique Mamberti alithibitisha utayari wa Kiti Kitakatifu, kuendelea
kusaidia Georgia katika siku zijazo. Pia uwakilishi wa Kiti Kitakatifu uliweza
kupewa taarifa mpya za maboresho yaliyofanya na serikali katika sera zake za mageuzi
katika uwanja wa ulinzi wa haki za binadamu. Askofu Mkuu Dominique Mamberti alirudia
kutoa misistizo katika kudumisha heshima kwa uhuru Georgia, uadilifu na sera mashirika
yasiyo tambuliwa bado kiserikali.
Pia Askofu Mkuu Dominique Mamberti alikutana
na Rais wa Georgia, Mheshimiwa Giorgi Margvelashvili, na Waziri Mkuu, Mr Irakli Garibashvili
na Spika wa Bunge, Mheshimiwa davit Usupashvili.
Aidha kati ya matukio ya
kukumbukwa katika ziara hii , ni Askofu Mkuu Mamberti , kuweka shada la maua katika
mnara wa Makumbusho ya watu waliofariki wakati wa machafuko ya kuleta Uhuru Georgia.
Na ameifunga ziara yake kwa kutembelea Khurvaleti. Jumapili Tarehe 14 Septemba, Ndani
ya mfumo wa ziara hiyo, Askofu Mkuu Dominique Mamberti alipokelewa na Mtakatifu na
Mwenyeheri Catholicos- Patriaki wa Georgia yote.