Upendo ni nusukaputi katika kusahihishana makosa-asema Papa
kusahihishana kikweli kidugu kunaweza kuwa kuchungu kwa sababu hufanyika kwa upendo,
ukweli na unyenyekevu. Kama wewe huko radhi kusahihishwa na ndugu yako, basi wewe
si mtu wa Mungu. Ni maelezo ya Papa Francisco mapema Ijumaa wakati akiongoza Ibada
ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta mjini Vatican, kama sehemu ya Maadhimisho
ya Sikukuu ya Jina Takatifu la Maria.
Maelezo ya Papa yalilenga katika somo
la Injili ambamo Yesu anawaonya wale wanaopenda kusahihisha makosa madogomadogo ya
wenzao na kuwa wachungu kusahihishwa dhambi zao kubwa, " ondoa kwanza boriti katika
jicho lako ndipo uweze kuona kibanzi katika jicho la ndugu yako.
Akizungumza
juu ya aya hizo za Injil, Papa Francisko pia alifanya rejea katika mahubiri yake ya
nyuma, juu ya ndugu kurekebishana, akisema ni muhimu kwa ndugu wapokosa, wakosolewa
au wasahihishwe lakini upendo. Alitolea mfano, ni vigumu kwa daktari kufanya upasuaji
katika mwili wa mtu bila nusukaputi. Ni jambo lisilowezekana vinginevyo mgonjwa atakufa
kwa maumivu. Vivyo hivyo , upendo ni nusukaputi inayomsaidia mtu kupokea tiba na
kukubali kusahihishwa,ni huduma na katika kukubali marekebisho. Na hivyo marekebisho
ni lazima yafanyike katika hali ya upendo, upole, unyenyekevu na majadiliano ya
kirafiki, isiwe kwa shutuma au ugomvi.
Pamoja na hilo, Papa aliongeza ni
lazima majadiliano hayo yafanyike bila kuupoteza ukweli hata kama ukweli huo unamwumiza
mtu. Ni lazima kusema ukwelI. Papa alieleza na kuhoji ni mara ngapi wanajumuiya wetu
wataeleza ukweli wa mambo ya mtu mwingine, na yale si ya kweli, uzushi, wenye kuharibu
sifa ya mtu huyo. Majadiliano - Papa alisema huumiza; na uvumi ni ni kiboko kwa sifa
za mtu, ni kichapo kinachoumiza moyo wa mtu. Ni wazi pia kwamba pale wanapoeleza
ukweli, si jambo la kufurahisha kusikia, lakini kama maelezo yanatolewa kwa matamshi
yenye upendo na urafiki, mtu huweza kukubali alichokifanya hata kama ni tendo la aibu,
kwa sababu anafahamu moyoni mwake kwamba ni kweli alifanya hivyo. Hivyo inakuwa tofauti
na kusingiziwa. Kwa maana hiyo, ni muhimu kusema ya kasoro za kweli za wengine kwa
moyo wa upendo.
Papa aliendelea kueleza kwamba, kurekebishana kidugu ni tendo
la uponyaji katika mwili wa Kanisa.Pale inapotokea uwepo wa shimo, katika kiambaza
cha Kanisa ni lazima kufanya ukarabati vinginevyo hatimaye ukuta mzima unaweza anguka.
Ni kufanya kama akina mama hasa mabibi wazee, wanavyofanya wakati wa kiziba matundu
yaliyojitokeza kwenye nguo, huziba tundu hilo polepole, na ndivyo inavyotakiwa katika
kurekebishana kidugu. Kama huna uwezo wa kufanya hivyo kwa upendo,ukweli na unyenyekevu,
nawe una makosa, una uharibifu ndani ya moyo wako. Huo ni unafiki na upofu ulioatajwa
na Yesu, mnafiki, kwanza ondoa pande la ubao katika jicho lako , ndipo uweze kukiona
kibazi kidogo katika jicho la nduguyo.
Papa aliasa, maneno haya, yasitutie
woga wa kusahihisha wengine iwapo tunaona dhahiri makosa ya wengine , inafaa kuwasaidia
kujirekebisha, kwa sababu ni muhimu kusahihishana kwa upendo, ukweli na unyenyekevu.
Na alimalizia homilia na wito wa kumwomba Bwana, daima tuweze kuubeba msalaba
mzito kwa ajili ya wema wa kusaidia wengine, tukiw tumejazwa na roho Mtakatifu na
upendo, upole na huruma yake. Tuombe ili tusiwe watu wa kuhukumu wengine, bali kusahihishana
katika hali ya udugu, upendo, kweli na unyenyekevu katika ukomavu wa kuwa wafuasi
wa Kristo. Bwana atusaidia katika huduma hii ya udugu, na uzuri wa kufanya hivyo
hata kama inaumiza, ili tuweze kuwasaidia kaka na dada zetu, kuyaisha maisha bora
ya utiifu, upendo, ukweli na unyenyekevu.