Hivi karibuni katika manisapaa ya kinondoni nchini Tanzania Shirika lisilokuwa la
kiserikali la WWF liiendesha mafunzo kwa wafanyakazi wa idara mbalimbali kuhusiana
na uenezaji wa hewa ukaa na matumizi ya nishati nchini. Mafunzo hayo yalitolewa
na Mtaribu wa Programu hiyo kutoka WWF Bi Teresia Olemako ambaye alitaja lengo la
mafunzo hayo ni katika kuhakikisha kuwa watumishi wa Idara mbalimbali wanakuwa na
ufahamu juu ya kukabiliana na madhara ya hewa ukaa na umuhimu wa kutumia nishati jadilifu. Aliongeza
kwakuwa mafunzo hayo yatahusu watumishi kutoka mikoa mitatu ambayo ni Dar es Salaam,
Kilimanjaro na Arusha kwasababu ni miji ambayoimeingia katika shindano la kimataifa
la kukabiliana na utunzaji wa mazingira ambalo litafanyika mwakani kwa kushirikisha
nchi 18 duniani Tanzania ikiwa ni mojawapo ya mshiriki kwa ikipata kwa mara ya kwanza. “WWF
kama shirika lisilo la kiserikali kwa ushirikiano na ICLEI linajipanga kusshirkiana
na watumishi wa miji iliyotajwa katika kuahakiksha kuwa suala la kupunguza hewa ukaa
na kuhimiza matumizi ya nishati jadilifu ni moja ya majukumu yao ambao nao watatumia
mafunzo hayo kuwapatia wananchi elimu Zaidi “aliongeza. Mtaribu huyo wa Programu
ya Nishatu Jadilifu alisema mradi huo utakuwa ukitambulika kwa kauli mbiu ya (Chakula,
Nishati, Taka Ngumu na Maji) kutumika kama njia mbadala ya kukabiliana na uharibifu
mazingira katika maeneo husika. Vilevile nishati jadilifu ikitumika ipasavyo itakuza
uchumi wanchi pamoja na wananchi kwa ujumla kutokana na ukweli kuwa haina madhara
na ipo kwa wakati wote hivyo ni vema kila mmoja kuwa balozi mzuri katika kuelimisha
jamii.