2014-09-09 07:43:24

Mafunzo kuhusu hewa ya ukaa Tanzania


Hivi karibuni katika manisapaa ya kinondoni nchini Tanzania Shirika lisilokuwa la kiserikali la WWF liiendesha mafunzo kwa wafanyakazi wa idara mbalimbali kuhusiana na uenezaji wa hewa ukaa na matumizi ya nishati nchini.
Mafunzo hayo yalitolewa na Mtaribu wa Programu hiyo kutoka WWF Bi Teresia Olemako ambaye alitaja lengo la mafunzo hayo ni katika kuhakikisha kuwa watumishi wa Idara mbalimbali wanakuwa na ufahamu juu ya kukabiliana na madhara ya hewa ukaa na umuhimu wa kutumia nishati jadilifu.
Aliongeza kwakuwa mafunzo hayo yatahusu watumishi kutoka mikoa mitatu ambayo ni Dar es Salaam, Kilimanjaro na Arusha kwasababu ni miji ambayoimeingia katika shindano la kimataifa la kukabiliana na utunzaji wa mazingira ambalo litafanyika mwakani kwa kushirikisha nchi 18 duniani Tanzania ikiwa ni mojawapo ya mshiriki kwa ikipata kwa mara ya kwanza.
“WWF kama shirika lisilo la kiserikali kwa ushirikiano na ICLEI linajipanga kusshirkiana na watumishi wa miji iliyotajwa katika kuahakiksha kuwa suala la kupunguza hewa ukaa na kuhimiza matumizi ya nishati jadilifu ni moja ya majukumu yao ambao nao watatumia mafunzo hayo kuwapatia wananchi elimu Zaidi “aliongeza.
Mtaribu huyo wa Programu ya Nishatu Jadilifu alisema mradi huo utakuwa ukitambulika kwa kauli mbiu ya (Chakula, Nishati, Taka Ngumu na Maji) kutumika kama njia mbadala ya kukabiliana na uharibifu mazingira katika maeneo husika. Vilevile nishati jadilifu ikitumika ipasavyo itakuza uchumi wanchi pamoja na wananchi kwa ujumla kutokana na ukweli kuwa haina madhara na ipo kwa wakati wote hivyo ni vema kila mmoja kuwa balozi mzuri katika kuelimisha jamii.








All the contents on this site are copyrighted ©.