2014-09-06 16:48:58

Siku Kuu ya Bikira Maria wa Upendo wa Cobre Cuba


Ujumbe wa Papa kwa maadhimisho ya Siku Kuu ya Bikira Maria wa Upendo wa Cobre Cuba. Jumamosi, Baba Mtakatifu Francisko alituma ujumbe wake kwa Askofu Mkuu Dionisio Guillermo García Ibáñez, wa Jimbo Kuu la Santiago de Cuba, ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Cuba, kwa ajili ya sherehe ya kitaifa ya kuienzi sanamu ya Bikira Maria wa Upendo wa Cobre hapo tarehe 8 Septemba, ambayo nakala yake imewekwa pia katika Bustani za Vatican.
Katika ujumbe huo Papa amesema, uwepo wake sanamu hiyo katika Bustani za Vatican, ni kumbukumbu inayoamsha hisia katika uhai wa Kanisa linalosafiri katika nchi za Caribbean kwa zaidi ya karne nne, ambalo kwa mara nyingine linakusanyka tena mbele ya Sura ya Mama wa Mungu, Mpendevu. Na sasa ni kutoka milima ya El Cobre, hadi kwa Khalfa wa Mtume Petro. Wana heri wale wanaopata muda hata kidogo wa kusimama katika madhabahu haya ya Maria, na kufanya ibada ya kuomba msaada wa kuongozwa nae, kumwelekea Yesu, Mwana wake.
Papa Francisco anaaendelea kusema, leo hii, kwa bidii tunaisherehekea Sikukuu hii ya Maria, Bikira wa "Mambisa," ambaye Wacuba wote, wameyageuza macho yao kwa Moyo wake Safi, kumwomba neema. Kwa ajili hiyo Papa, ametoa pongeza kwa wapendwa hao wote, huku akiwataka waige unyenyekevu wake na uaminifu wake kwa Kristo, ambavyo sharti la kwanza la mwanafunzi bora wa Yesu.
Na kwamba, yeye Papa kila mara anaposoma maandiko matakatifu, ambamo Bwana anaongea na anaongea ya Mama yetu, hupatwa na mawazo katika maneno matatu: shangilia, uamka na uvumilia.
Papa ameelezea kushangilia, akisema lilikuwa ni neno la kwanza la Malaika Gabriel kwa Bikira Maria, “Salaam, umejaa neema, Bwana yu pamoja nawe" (Lk 1:28).Na hii inaonyesha maisha ya mtu aliyemgundua Yesu, ni kujazwa na furaha ndani, kwamba hakuna kitu chochote na hakuna mtu anaweza kuinyakua furaha hiyo. Na ndivyo ilivyo kwa Wakristo wa Cuba katika Siku Kuu hii, wanafurahi kwa sababu ya kuwa ya uwepo wa Bikira wa Upendo, anayetoa mwaliko kwa watu wote, kuishi kwa upendo wa kweli, na si kuanguka katika mitego mibovu ya maisha ya jicho kwa jicho - jino kwa jino. Ni furaha iliyoje kusikia yupo mmoja mwenye kuwa na upendo wa kweli, pamoja na ukweli wa maisha, na si ya wale wenye kutoa maneno matupu, yenye kupeperushwa mbali kwa upepo.
Papa pia amelizungumzia neno la pili, amka akirejea Injili ya Mtakatifu Luka, ambamo Maria aliamka na kwenda kumsaidia binadamu yake Elizabeth, ambaye katika uzee wake alikuwa akisubiri kuzaa mtoto (Luka 1: 39-45). Hii ilikuwa ni kutimiza mapenzi ya Mungu, kwa wale wanaohitaji. Maria alifikiria juu ya matatizo ya wengine na kujitolea kuwasaidia. Huu ni ushindi mwingine wa Maria, ananyanyuka na kwenda kusaidia mhitaji. Na ndivyo nasi pia tunahitaji, kuwa tayari kusaidia wahitaji wenye shinda. Tunahitaji kumwiga Maria bila kukata tamaa katika kuubeba mzigo wa wengine kama wajibu wetu. Na haya si mambo makubwa,iwapo tutafanya hivyo kwa upendo unaotoka ndani ya maisha yaliyobadilishwa na Yesu, kufanya kila kitu kwa huruma. Maria daima anafanya hivyo, yuko karibu na watu wake, katika neema ya watoto. Yeye aujua upweke, umaskini na hata maisha ya uhamishoni, na amejifunza jinsi ya kujenga udugu na kufanya sehemu yoyote, kuwa mahali pazuri pa kukaa. Na tumwombe atupe roho ya mtu maskini ambaye hana kiburi, moyo safi wenye kumcha Mungu, bila kurudishwa nyuma na ugumu wa maisha.
Na neno la tatu ni tumaini. Maria, ambaye ana uzoefu wa wema wa Mungu, alitangaza ukuu kwamba alio mfanyia (Luka 1, 46-55). Maria hakuzitumainia nguvu zake mwenyewe, lakini katika Mungu, ambaye upendo wake hauna mwisho. Kwa hili, alibaki na Mwanae , na Mitume wake bila kupoteza tumaini. (Matendo 1:14). Na ndivyo nasi pia tunaitwa kubaki katika upendo wa Mungu na kukaa katika upendo wa wa kuwaelekea wengine, katika dunia hii yenye matatizo mengi, bila ya kupoteza tumaini. Papa alikamilisha ujumbe wake kwa kuwataka wana wa kanisa Cuba pia wamkumbuke katika sala zao.








All the contents on this site are copyrighted ©.