2014-09-06 09:43:34

Papa: hakuna sababu za kuhofia mabadiliko katika Kanisa


Papa Francisco mapema Ijumaa alitoa wito kwa waumini wote kutohofia mabadiliko ndani ya Kanisa, kwa kuwa, ujumbe wake wa Injii ni habari njema, ambamo Yesu anatutaka kuachana na miundo ya maisha isiyofaa tena. Papa alitoa rai hiyo wakati akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la ndani ya Vatican.

Alisema kuwa, Mkristo hapaswi kuwa "Mtumwa wa sheria nyingi ndogo ndogo ", lakini ni kuufunua moyo wake kwa amri mpya ya upendo.
Papa alisema hilo kwa kutazama unafiki wa waandishi mafarisayo, walivyofikiri wanaweza kumdhihaki Yesu kwa kumwuliza maswali kwa kejeli kama kwa nini wanafunzi wake hawafungi. Lakini Bwana alitambua hilo na kuwapa majibu yaliyowafanya watazame chini kwa aibu.

Papa pia alifafanua ujumbe wa Injili katika mfano wa “Mvinyo mpya, viriba vipya” akisema, hii ni habari ya furaha kwamba, walimu hawa wa sheria walikuwa wamefungwa katika amri za maagizo yao. Hata Mtume Paulo anasema, kabla ya ukombozi wa Yesu, wote walikuwa wafungwa chini ya sheria. Papa alisema, sheria za watu hao si kwamba zilikuwa ni mbaya, zilisaidia kuwalinda, lakini kwa kuwaweka kama wafunga wa sheria katika mtazamo wa imani. Sheria nyepesi ya Yesu ya Upendo, iliweza kuwafungua waumini dhidi ya sheria hizo nyinginyingi. Imani iliyowekwa wazi zaidi na Yesu mwenyewe.

Papa alieleza na kuhoji iwapo Ukristo una sheria na alitoa jibu “Ndiyo”. Yesu alisema: 'Mimi sikuja kuifunga sheria, lakini kuikamilisha katika ukamilifu wake. Na ukamilifu wa sheria, kwa mfano, umo katika sheria ya Upendo na Heri za Mlimani,zilizotajwa na Yesu, na kama alivyotupenda. Na wakati Yesu anawakemea walimu hawa wa sheria, ni kwa kuwa washindwa kuwasaidia watu kuzielewa sheria badala yake waliwafanya kuwa watumwa wa sheria nyingi, katika mambo madogo madogo mengi, yakiwa si ya lazima kufanya hivyo.

Na sasa nini cha kufanya, aliongeza, kwa uhuru ulioletwa na Yesu, unatuongoza katika ukamilifu wa sheria yake mpya, sheria aliyoikamilisha kwa damu yake mwenyewe. Na hili ni upya wa Injili, yenye kutupa mpumuo wa furaha ya kweli na uhuru. Na ndiyo maana ya mvinyo mpya na na viriba vipya. Na hivyo tusiwe na woga wa kufanya mabadiliko kwa mujibu wa sheria ya Injili.


Papa Francisco mapema Ijumaa hii alitoa wito kwa waumini wote kutohofia mabadiliko katika Kanisa, kwa kuwa Injii ni Ujumbe , na Yesu anatutaka kuachana na miundo isiyofaa tena. Papa alitoa rai hiyo wakati akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la ndani ya Vatican.
Papa alisema kuwa, Mkristo hapaswi kuwa "Mtumwa wa sheria nyingi ndogo ndogo ", lakini ni kuufunua moyo wake kwa amri mpya ya upendo. Papa alisema hilo kwa kutazama jinsi Waandishi mafarisayo walivyofikiri wanaweza kumdharirisha Yesu kwa kumwuliza maswali magumu kama kwa nini wanafunzi wake hawafungi. Lakini Bwana anatambua mtego wao na kuwapa majibu yaliyowafany akwatazame chini kwa aibu.
Papa pialaifafanua ujumbe wa Injili katika mfano wa “Mvinyo mpya, viriba vipya” ulioandikwa katika Injili akisema, hii ni habri ya furaha kwamba, walimu hawa wa sheria walikuwa wamefungwa katika amri za maagizo yao. Hata Mtume Paulo anasema, kabla ya ukombozi wa Yesu, wote walikuwa wafungwa chini ya sheria. Papa alisema, sheria za watu hao si kwamba zilikuwa ni mbaya, ziliwalinda lakini kwa kuwaweka kama wafunga katika mtazamo wa imani. Imani hiyo iliyowekwa wazi zaidi na Yesu mwenyewe.

Papa alieleza na kuhoji iwapo Uristo hauna sheria na alitoa jibu la “Ndiyo”. Yesu alisema: 'Mimi sikuja kuifunga sheria, lakini kuikamilisha katika ukamilifu wake. Na ukamilifu wa sheria, kwa mfano, ni Heri alizohubiri Yesu Mlimani, sheria ya upendo, upendo jumla, kama Yeye - Yesu - alivyotupenda. Na wakati Yesu anawakemea watu hawa, hawa madaktari wa sheria, sanawakemea kwa kushindwa kuwasaidia watu kuzielewa sheria badala yake wanawafnya kuwa watumwa wa sheria nyingi katika mambo madogo madogo mengi, yakiwa si ya lazima kufanya hivyo.
Na sasa nini cha kufanya, aliongeza, ni kwa uhuru ulioletwa na Yesu unaotuongoza katika ukamilifu wa sheria yake mpya, sheria aliyoikamilisha kwa damu yake mwenyewe. Na hii ni upya wa Injili, yenye kutupa mpumuo wa furaha ya kweli na uhuru. Na hivyo ndiyo maana ya mvinyo mpya na na viriba vipya. Na hivyo tusiwe na woga wa kfuanya mabadiliko kw amujibu wa sheria ya Injili.








All the contents on this site are copyrighted ©.