Ghasia za Ukraina Bado kuna wasiwasi mkubwa unaondelea nchini Ukraina
kwa sababu ya mapigano katika maeneo ya mashariki ya mji mkuu Kiev. Waziri wa
ulinzi wa Ukraina Bwana Valeri Gheletei aliandika kuwa nchini Ukraina imeingia vita
kubwa ambavyo havijawahi kuonekana Ulaya, ambavyo tayari imesababisha makumi na maelfu
ya watu kupoteza maisha.. Wanajeshi wa Ukraina waameacha uwanja wa ndege wa Lugansk
chini ya ulinzi waasi wa Kirusi. Ni vigumu kuhesabu waliokufa kutoka Kiev, inadaiwa
wanajeshi saba kufariki na wengine 25 majeruhi, katika muda wa saa 24, wanajeshi 260
wametekwa na kufungwa kama wafungwa wa kivita baada ya mapigano makari katika mikoa
ya Donetsk. Pamoja na hali hii inayoendelea kumefanyika mkutano kati wa wawakilishi
kutoka Urusi, Ukraina , Osce na kutoka katika kikundi la waasi ambao walitengana
na Urusi wakidai kutambuliwa hali zao kwa namna ya pekee kwenye mikoa ya mashariki
ya Ukraina. Na mkutano mwingine wa unategemewa kufanyika 5 Septemba 2014. Pamoja
na hayo yote bado kuna utata katika kupata ufumbuzi wa tatizo la nchi hizo mbili
kwa na hivyo kutia wasiwasi mkubwa Muungano wa nchi za ulaya ambao bado unatafuta
suluhu. Hayo yalielezwa na Bwana Donald Tusk huko Danzica, Mwenyekiti wa Ushauri
wa nchi za Ulaya katika kuadhimisha kumbukumbu ya kuanza kwa vita vya pili vya dunia
iliyoadhimishwa hivi karibuni. Bwana Donald Tusk alisema kuwa wasiwasi wake ni kwamba
ipo hatari ya kurudiwa tena vita vile vilivyotokea Septemba 1939.
ITALIA Shirika
la habari la Ansa limeripoti kwamba katika Mkutano Mkuu wa Baraza la Ulaya ,lilifanyoka
hivi karibun huko mjini BRUXELLES limewateua wajumbe wake wawili Donald Tusk wa
Poland, nao ni Mwenyekiti wa kudumu wa Baraza la Ushauri la nchi za Ulaya na Mikutano
yake Mikuu , na Waziri wa mambo ya nchi za nje Federica Mogherini wa Italia, kuwa
wawakilishi Katika Muungano wa nchi Ulaya katika masuala ya siasa za nje na ulinzi. Pia
suala la Ukraina lilijadiliwa katika Mkutano Mkuu wa Baraza hilo la Ulaya, ambamo
Bwana Tusk , alilizungumzia akisema kwamba nia kuu Umoja wa nchi za Ulaya ni kufikia
amani , ambayo itatokana na juhudi makini za wale walioandaliwa kufanya hivyo na ya
kwamba ana uhakika mkubwa kuwa jinsi ilivyojitokeza kwa kipindi kilichopita , Muungano
wa ulaya utatafuta njia za kuweza kufikia muafaka wa pamoja katika lengo hilo la amani
Ukraina. Naye Federica Mogherini Mwakilishi wa siasa za nje na ulinzi na Waziri
wa nchi za nje nchini Italia aliongezea kusema Ulaya ina changamoto kubwa sana lakini
anawashukuru na kuwapongeza viongozi hawa kwa imani kuu waliyo nayo. Viogozi hawa
waliochaguliwa wametanguliza kazi ya kutafuta amani kuwa kipaembele cha juu msingi.
Rais Jamhuri ya Italia Bwana Giorgio Napolitano alimpongeza waziri wa nchi za
nje Mogherini kwa kuteuliwa kwake, na pia Waziri mkuu wa nchi ya Italia Renzi alimtakia
kazi njema aliyokabidhiwa.
Libia: Wizara ya serikali za mitaa Libya
yatekwa na wapiganaji Libya imekumbwa na ghasia tangu kuagushwa mamlakani
ya hayati kanali Muammar Gaddafi aliyepinduliwa na wanajeshi wa Nato wakisaidiwa na
wapiganaji wa kiisilamu mwaka 2011. Taarifa zilizotoka katika serikali hiyo zinasema
kuwa ,Watu waliokuwa wamejihami waliwazuia wafanyakazi kuingia katika ofisi za wizara
hiyo. Na pia Jumapili 31.08.2014, wapiganaji hao waliteka makao ya ubalozi wa Marekani,
hawa ni wakipiganaji miongoni mwao wenyewe wanao tafuta mamlaka. Maafisa wakuu
wa serikali na wabunge walihamia katika mji wa Tobruk, Mashariki mwa nchi hiyo mwezi
uliopita. Marekani na mataifa mengine yalilazimika kuwaondoa wafanyakazi wao kutoka
nchini humo mwezi Julai huku mapigano yakizidi kuwa makali mjini Tripoli. Taarifa
zinaendelea kueleza kuwa Waziri mkuu Abdullah al-Thinni na baraza lake la mawaziri,
walijiuzulu wiki iliyopita ili bunge liweze kuteua serikali mpya. Nchini Libia
viongozi wa hawamu hiyo walikuwa niwa uchaguzi wa pili tangu kanali Gaddafi kuuawa
katika mapinduzi yaliyotokea ya mwaka 2011. Kutokana na ghasia zinazoendelea
huko Libya , hata Shirika la habari la Fides limemkariri Balozi wa Papa Martinelli
nchini Libia mji Mkuu Tripol akisema kuwa hali sasa inaendelea kuwa shwali , kuna
utulivu kidogo kwani mabomu yametulia kulinganisha na siku zilizopita. Ni matumaini
yake kuwa neema ya Mungu inaweza kusadia hali iweze kuendelea hivyo kwa utulivu Balozi
anasema kwamba hadi sasa wamepata matatizo makubwa na hasa jumuiya ya wakristo,. Watu
hawa hata kama ni wachache wanakwenda kanisa kwasababu ni furaha ya kukutana. Mon
Martinelli anaongeza kuwa, tarehe 5Septemba ni sikuu ya Mama Teresia wa Kalkuti,
wanategemea watafika watu katika sikukuu hiyo. Anamalizia kusema kuwa watu waendelee
kuiombea nchi ya Libia hili iweze kupata amani.
AFRIKA YA KUSINI:RAIS
JACOB ZUMA AFANYA MKUTANO WA DHARURA N Jumamosi Sept 30 Jeshi lilizingira
makao ya waziri mkuu na kumlazimu kukimbilia nchini Afrika Kusini pamoja na mawaziri
wake. Inaarifiwa kuwa jeshi lilikuwa linamzuia waziri mkuu kumfuta kazi mkuu wa majeshi. Hata
hivyo jeshi limekanusha madai hayo likisema lilipokea taarifa kuwa polisi walikuwa
wanapanga kuhami vikundi vya vijana ambao wangefanya maandamano kulazimisha waziri
mkuu kufungua vikao vya bunge. Maandamano hayo hayo lakini yalisitishwa. Wakati
huo Serikali ya Afrika Kusini ambako waziri mkuu huyo amepata hifadhi, imesema haitastahamili
mapinduzi kufanyika katika nchi hiyo. Inaonekana kulikuwa na njama ya mapinduzi
nchini humo, lakini jeshi linasema kila kitu kiko shwari. Baadhi ya viongozi wa kanda
hiyo,wamefanya mkutano kujadili hatua watakazochukua, ambapo Jumapili usiku ulifanyika
mkutano huo wa dharura kati ya Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma na waziri mkuu wa
Lesotho, Thomas Thabane, Mkutano huo ulilenga kutafuta nyenzo za kumaliza mgogoro
wa kisiasa katika ufalme huo mdogo.Mawaziri wa ulinzi na mambo ya nje wa Namibia na
Zimbabwe walishiriki kwenye mkutano huo ingawa taarifa zaidi zilizojadiliwa kwenye
mkutano huo bado hazijatolwa.
UZINDUZI MPYA WA KUKATA TIKETI TANZANIA
Meneja Mkuu wa Travelport, Eliasaph Mathew ameishauri Serikali ya Tanzania kupunguza
kodi katika huduma za usafiri wa anga ili watanzania wengi wamudu kuutumia usafiri
huo katika shughuli zao za kiuchumi. Ushauri huo umetolewa Mosi September wakati
wa uzinduzi wa mtandao mpya wa ukataji wa tiketi za ndege uitwao (PreciseSky), utakaosaidia
mashirika madogo ya ndege kuhimili ushindani wa biashara ya usafiri wa anga. Trevelport
ni kampuni ya kimataifa inayojihusisha na kuyapatia mashirika ya ndege duniani mifumo
ya ukataji wa tiketi. Meneja huyo alisema kuwa “Hii inadidimiza uchumi kwa sababu
mtalii anaona heri aende Uganda au Kenya anakotozwa kidogo wakati Tanzania ndiyo mojawapo
ya vivutio vingi zaidi vya utalii kulinganisha na nchi za Afrika Mashariki, sasa
hivi tena wanapendekeza VAT iwekwe kwenye usafiri wa anga”. Aliongeza “… Nayo hiyo
itadhohofisha biashara katika usafiri wa anga maana hakuna nchi yeyote duniani inayotoza
VAT sekta ya usafiri wa anga,” Aliendelea keleza kuwa hivi sasa watumiaji wa
usafiri wa anga duniani wanapata mahitaji yao kupitia mitandao ikiwemo ununuzi wa
tiketi, sehemu ya kukaa kwenye ndege, chakula na hoteli wanazotaka kufikia kwenye
nchi wanazokwenda hivyo kuna haja kwa makampuni yanayotoa huduma kwenye sekta hiyo
kwenda na wakati. Pia Meneja wa mtandao huo mpya wa Precise Sky, Gloria Urasa
alisema mfumo huo ni mpya Tanzania na utayasaidia mashirika madogo ya ndege hapa nchini
kuonekana duniani kwa kuongeza sehemu za kuuzia tiketi za ndege zao hivyo kuzidi kukua
kibiashara.