2014-08-30 10:10:55

Wakristo Gaza wauishi wito wa Papa :Kuweni Chumvi na Mwanga wa dunia


Padre Jorge Hernandez, mmishonari wa Taasisi ya Neno Aliyefanyika Mwil, ambaye ni Paroko katika Parokia ya Gaza, akizungumza na Redio Vatican Radio, Ijumaa iliyopita alieleza kwamba , Ujumbe wa Papa aliowaachia Wakristo wa Gaza, umekuwa muhimu katika kuwaunganisha, licha ya kukabiliwa nahali ngumu kama Wakristo wanaoishi katika eneo hilo. Na tena wakati wa machafuko, hufarijika kwamba, Papa yu karibu nao siku zote.

Padre Hernandez aliiambia Redio Vatican, baada ya kukutana na Papa Francisco, kukutana aliko kuita neema na baraka kubwa kwake, ingawa haikuwa mara ya kwanza. Katika mazungumzo yao, Papa Francisco aliendelea kutia moyo Jumuiya ndogo Katoliki ya Gaza, akiitaka idumu na iendelee kuwa “chumvi ya dunia katika nchi ya Gaza. Na kwamba Yeye pia amekuwa akiguswa na ujumbe wa ushuhuda unao tolewa na Papa kwa Kristo. Na ndivyo pia jumuya ya Wakatoliki Gaza,wanauishi wito wa Papa kama wito maalum katika kumshuhudia Yesu Kristo katika nchi yao, ambayo ni nchi ya Yesu, kama nyumbani, nchi iliyo shuhudia mateso na kifo na ufufuko wake Kristo.

Gaza ina wakazi wapatao karibia milioni mbili. Jumuiya ya Wakristo ni ndogo sana, wakiwa jumla 1,300 kati yao Wakatoliki ni 136. Na uhusiano kati ya Wakristo ni mzuri sana.
Padre Hernandez alisema, uwajibikaji wa Papa Francisko kwa Wakristo wa Gaza, imekuwa ni sementi inayowaimarisha kiimani na katika kuwafariji, hasa katika kumshuhudia Mkuu wa Amani Yesu Kristo.
Na kwamba, watu wa Gaza wanatumaini, amani iliyopatikana sasa kati ya vikosi vya Israel na Palestina, itakuwa ya muda mrefu. Watu wote wamechoka na vita, wamechoka na mateso. Na sasa inaonyesha wengi kupata ufahamu kwamba, hakuna anayeweza kufanikiwa iwapo kuna vita. Kila upande huathirika kwa njia moja au nyingine. Na hatima yake, hakuna anayefaidika kutokana na vita, wote hupoteza.

Padre Hernandez anatumaini kwa baraka za Mungu, wataendelea kuwa na nguvu za kuanza tena maisha mapya. Na ili kujenga amani ya kudumu, Padre Hernandez alisisitiza ni lazima kujenga amani na haki. "Amani inahitaji kujitoa sadaka, na inawezekana.

Na alitumia muda huu wa kuzungumza na Redio Vatican , kutoa shukurani zake kwa watu wote duniani ambao wamekuwa karibu na jamii yake, hasa katika kipindi cha majaribu katika wiki za hizi karibuni. Muda ambao umekuwa mugumu na ambamo waliyatolea mateso yao kama sadaka katika kuombea amani hasa kwa ajili ya wagonjwa. Alibainisha idadi kubwa ya Wakristo katika Parokia yake ya Gaza, mara nyingi hutolea sala, misa na ibada zingine kwa nia za kuwakumbuka wale wanaoomba pia kwa ajili yao. “Nataka kuchukua fursa hii," alisema, "kusema asante, na Mungu akubariki."








All the contents on this site are copyrighted ©.