Maaskofu Katoliki Kenya watoa tamko lao juu ya hali ya taifa.
Baraza la Maaskofu Katoliki nchini KenyA(KCCB), Alhamisi Agosti 28, kupitia Tume
yake ya Haki na Amani, lilitoa tamko lake lenye jina, "Uwajibikaji wa Viongozi katika
Umoja na Usalama wa Nchi Yetu”mbele ya mkutano wa vyombo vya habari, katika mtazamo
wa kutoa mwanga katika kile kinachoendelea ndani ya marubano ya kisiasa nchini Kenya.
Maaskofu walitoa tamko lao kwa wanahabari baada ya majadiliano yao katika mkutano
wao wa mwaka uliofanyika Kwale katika Jimbo Kuu la Mombasa. Tamko hilo, limeangalishwa
katika Injili ya Luka12:28 “Na kila aliyepewa vingi kwake, huyo vitatakiwa vingi,
naye walimwekea amana vitu vingi , kwake huyo watataka na zaidi".
Tamko la
Maaskofu limeanza na salaam za rambirambi za dhati kwa familia za wahanga na watu
wa Kata ya Mandera, ambako kulifanyika mauaji ya hivi karibuni na migogoro baina ya
koo ambavyo vinamesababisha uharibifu mkubwa wa maisha na mali. Na kwamba , kama Tume
ya Amani, wana wasiwasi na kujali uwepo wa mfumo au utaratibu wa kutoa silaha za moto
kwa makundi mbalimbali wanamgambo, na hasa uhamasishashi wa ubabe kwa makundi ya vijana,
migogoro na mauaji mengi, yanayofanyika katika makazi ya watu na uharibifu wa mali
, kama inavyo shuhudiwa katika Wilaya mbalimbali. Maaskofu wanasema uhalifu huu wa
kutisha halikubaliki kabisa. Kila maisha mtu yana thamani isiyoweza kuwa na mbadala.
Nahivyo wamezitaka pande zote kuacha utamaduni huu wa kifo. Na kwamba chuki na fitina
za kutaka kulipiza kisasi, "Jicho kwa jicho” ni kuleta tu upofu wa kuendeleza vurugu.
Hivyo Maaskofu wanasema, wakati umefika kwa Wakenya kuona umuihimu wa kuachana
na matendo yasiyokuwa na maendeleo, badala yake wajihusishe zaidi katika utendaji
kwa maslahi ya taifa na si kwa maslahi ya mtu binafsi au makundi ya kisiasa . Viongozi
wote wanatakiwa kuhamasisha utendaji wa mazuri kwa manufaa ya watu wote wa Kenya.
Wakenya
kwa masikitiko walishuhudia mapambano makubwa ya wanasiasa wakati wa uchaguzi katiak
ngazi zote , tangu madiwani, wabunge, Maseneta, Wanawake Wawakilishi, Magavana na
viongozi wa kitaifa kwa gharama watu wa Kenya. Na kwamba Tume Katoliki ya haki na
amani, ina ufahamu wa mizizi ya kihistoria katika masuala ya ardhi Kenya. Jambo
hili imebakia kitendawili kwa kila jaribio la serikali inayopita huliacha bila kupta
suluhu. Kwa hiyo, Tamko la Maaskofu limetoa mapendekezo yake kama ilivyoshauriwa
na Tume Katoliki ya haki na amani katiak yafuatayo kwamba tabaka la wanasiasa, ni
lazima kujenga mashauriano na uelewa juu ya suala la kura ya maoni ili kuhakikisha
kwamba ni kwa ajili ya maslahi ya Wakenya na si kutumikia maslahi yao wenyewe.
Na
juu ya suala la ardhi, serikali na taasisi zake lazima kutekeleza mfumo wa kina kama
ilivyo elekezwa katika Katiba ya Kenya, 2010 na sheria ya baadae juu ya nchi, na hivyo
Serikali inapaswa kutekeleza mapendekezo ya Ripoti ya Ndung'u na ripoti ya Tume ya
Ukweli, Haki na Maridhiano.
Tamko linawakumbusha Wakenya wote kwamba, ulinzi
na usalama ni wajibu wa kila mtu. Suala la usalama halina mzaha. Viongozi wote wa
chama tawala cha muungano na upinzani ni lazima kuungana na kutenda kwa pamoja ili
nchi idumu katika hali ya usalama na amani. Kwa maana hiyo kila kiongozi aliyechaguliwa
na wananchi ni lazima atimize wajibu wake kwa mujibu wa Katiba katika kuwatumikia
Wakenya na kuondokana na ushindani wa kung’ang’ania madaraka katika uwanja wa kisiasa.
Pia
tamko la Maaskofu limeonyesh akujali ukosefu wa ajira kwa vijana, kwamba inaendelea
kubaki tishio kwa usalama! Kwa hiyo ni lazima jitihda zaidi zifanyike kupata ufumbuzi
wa tatizo hili iwe kimafunzo au katiak juhudi za maendeleo. Na utawala ni uwe mstari
wa mbele katiak kuhakikisha ushiriki wa wananchi katika masuala ya maendeleo.
Na
mwisho tamko linatoa wito kwa Wakenya wote, kuwa mlizi wa mmoja kwa mwingine, kw akuwa
taifa la Kenya ni rasilimali yao wote , nahivyo ni lazima kutumia vyema na kuilinda. Mungu
ibariki Kenya. Tamko limetiwa na Saini na: Askofu Mkuu wa Kisumu na Mwenyekiti
wa Tume ya Haki na amani ya KCCB – Askofu Mkuu Zakayo Okoth; Askofu i Cornelius Korir,
wa Jimbo la Eldoret ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti waTume Katoliki ya Haki na amani
KCCB; Askofu wa Machakos na Mjumbe wa Tume, Askofu Martin Kivuva Musonde, pamoja
na wawakilishi kutoka Chama kinachounganisha Mashirika Katoliki ya Masista Kenya
(AOSK) na mwakilishi kutoka mwavuli unaouganisha Wakuu wa Mashirika ya Kidini Kenya
(RCSK).