Wanajeshi 480 wa Nigeria wametorokea maisha yao nchi jirani ya Cameroon kufuatia makabiliano
makali dhidi ya wapiganaji wa kundi la kiislamu la Boko Haram. Msemaji wa jeshi
la Cameroon Luteini Kanali Didier Badjek amethibitisha kisa hicho na kusema kuwa
wamepokonywa silaha na sasa wamewekwa katika shule .Mapigano hayo yanaendelea karibu
na mji ulioko mpakani wa Gamboru Ngala.Mapigano hayo yanawadia saa chache tu baada
ya wapiganaji hao wa Boko Haram kutoa kanda ya video ambayo walitangaza kuundwa kwa
himaya ya Kiislamu kaskazini Mashariki mwa Nigeria. Kiongozi wa Boko Haram Abubakar
Shekau alizungumza kwenye kanda ya video iliyotolewa ili kupongeza wapiganaji wake
kwa kuchukua udhibiti wa mji wa Gwoza mapema mwezi huu.Lakini haijabainishwa iwapo
Bwana Shekau ameahidi kutii Muungano wa wapiganaji wa kundi la kiislamu la Islamic
State inayotawala sehemu kubwa ya Kaskazini mwa Iraq na Syria.