2014-08-27 09:24:25

Albania yajiandaa kwa ujio wa Papa Francisko


Baba Mtakatifu Francisko, anatazamia kufanya ziara ya Kichungaji ya siku moja nchini Albania mwezi ujao Septemba, kwa lengo la kuhamasisha mshikamano na umoja wa kitaifa kwa nchi hiyo ambayo kwa muda mrefu iliteswa na utawala wa udikteta wa kikomunisti, uliowatenga pia wananchi wake na nchi zingine duniani.

Albania, nchi ya kuzaliwa ya Mama Mtakatifu Tereza wa Calcutta, katika miaka ya 1990, makumi ya maelfu ya maskini wa Albania, walikimbilia Italia, wakivuka Bahari ya Adriatic katika vyombo hafifu vilivyo hatarisha maisha yao, zikiwemo boti za wavuvi. Watu walikimbia mateso na dhuluma zilizokuwa zikifanywa na utawala wa wakati huo, wengi wao walipokelewa na kuingizwa katika maisha ya Italia.

Papa Francisco wakati wa sala ya Malaika ya Jumapili moja, aliwaambia waamini waliofika kusali katika uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro kwamba, ana hamu ya kuitumia ziara yake Septemba 21 Albania, walau kutoa msaada mdogo kwa jamii Katoliki maskini wa Albania.

Theluthi mbili ya raia wa Albania wapatao milioni 3.2 ni Waislamu ambao huishi kwa amani na kundi dogo Orthodox, Katoliki. wakati wote wa utawala wa kidikteta wa kikomunisti kati ya mwaka 1967-1990, hawakuwa na utendaji wowote wa kidini katika maisha ya kijamii.

Waziri Mkuu Kialbeni Edi Rama amesema ziara ya Papa Itasaidia kukuza maadili hasa kujenga ushirikiano na amani miongoni mwa watu wa imani na makabila mbalimbali . Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Albania kutembelewa na Papa, mara ya kwanza lilitembelewa na Papa Yohane Paulo II, baada ya kuangushwa kwa utawala wa kikomunisti mwaka 1993.
Nchi ya Albania ina ukubwa wa eneo km ² 28,748 ,Idadi ya Watu milioni 3.250, ambao kati yao Wakatoliki ni 517,000 wanaohudumiwa na Majimbo 6 yanayundwa na Parokia 124 na vigango 25 . Kuna Maaskofu 8 , Mapadre wa Jimbo 54, Mapadre Watawa 93 , Mashemasi wa kudumu 2 , Mabruda 16, Masista 478, Wamisionari walei 36 na Makateksta 331.
Kuna shule za msingi 54, sekondari sekondari 14 – taasisi za masomo ya juu na vyuo vikuu 5. Hospitali 8, Zahanati za upasuaji 29 na nyumba kwa ajili ya wazee au walemavu 16, Yatima 16 .








All the contents on this site are copyrighted ©.