Baba Mtakatifu Francisko, wakati wa Katekesi yake, Jumatano tarehe 20 Agosti 2014,
amewashukuru wale wote waliomtumia salam za rambi rambi kutokana na msiba ulioikumba
familia yake kutokana na ajali ambayo imesababisha Mpwa wake kupoteza mke na watoto
wawili. Ajali hii imetokea nchini Argentina. Salam hizi za rambi rambi zimesomwa wakati
wa Katekesi yake katika lugha mbali mbali.
Baba Mtakatifu amewakumbusha mahujaji
ya wageni waliokuwa wamemiminika kwa wingi mjini Vatican ili kusikiliza Katekesi yake
mara baada ya kujerejea kutoka katika hija ya kitume nchini Korea ambako amehudhuria
maadhimisho ya Siku ya Sita ya Vijana Barani Asia pamoja na kuwatangaza Mashahidi
124 kutoka Korea kuwa ni Wenyeheri.
Baba Mtakatifu anasema wao katika familia
yao walikuwa watoto watano. Kwa sasa ana wapwa zake kumi na sita na kati yao, mmoja
wao amempoteza mke na watoto wawili na yeye mwenyewe hali yake bado si nzuri. Anasema
hata Papa anafamilia. Amewaambia mahujaji kwamba, ni mshabiki mkubwa wa Timu ya Soka
ya San Lorenzo ambayo hivi karibuni ilitwaa ubingwa.
Timu hii anasema, ni
sehemu ya utambulisho wake wa kitamaduni. Baba Mtakatifu Francisko amebahatika kusalimiana
na wachezaji wa timu hii mmoja mmoja pamoja na kupiga nao picha ya pamoja wakiwa wamebeba
Kombe la ushindi.