2014-08-20 11:56:41

Jitihada za Umoja wa Mataifa katika kupambana na Ebola


Bwana David Nabarro, mtaalam na mkurugenzi wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia ugonjwa wa Ebola ambao kwa sasa umekuwa ni tishio, Siku ya Jumatano tarehe 20 Agosti 2014 anaondoka mjini Washington DC, Marekani kuelekea Afrika Magharibi ili kusaidia juhudi za kupambana na ugonjwa wa Ebola. Akiwa Afrika Magharibi anatarajiwa kuzungumza na wananchi, jumuiya na viongozi wa Serikali ambazo zimeathirika kwa ugonjwa wa Ebola.

Bwana David anasema amekwishazungumza na Benki ya Dunia, wataalam wa kudhibiti na kutibu magonjwa ya mlipuko kutoka Serikali ya Marekani pamoja na wadau wengine, ilikuhakikisha kwamba, Umoja wa mataifa unawasaidia wananchi wa Afrika Magharibi kukabiliana kikamilifu na ugonjwa wa Ebola. Akiwa Afrika Magharibi Bwana David anatarajiwa kutembelea Liberia, Sierra Leone, Guinea na Nigeria.

Hizi ni nchi ambazo kwa sasa zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa wafanyakazi katika sekta ya afya, lakini zaidi kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Ebola pamoja na kuwatunza wagonjwa wengine pia.







All the contents on this site are copyrighted ©.