2014-08-19 10:58:49

Papa akamilisha ziara yake Korea


Jumatatu, mara baada ya Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu la Myeong –dong, Baba Mtakatifu aliekea katika uwanja wa ndege wa Seoul, ambako aliagana na wenyeji wake, Rais Park Geun-hyne, Nunsio wa papa nchni Korea, Mons. Oswald Padila Maofisa a ngazi za juu katika wa utawala wa Jamhuri ya Korea Kusini, wakiwalikisha utawala wote mahalia.
Papa aliagwa kwa gwaride la heshima la kijeshi kabla ya kupanda ndege ya Shirika la Korea kuelekea Roma, akiwa amekamilisha ziara yake ya siku tano nchini Korea Kusini. Jumatatu hii Papa na ujumbe wake, alitarajia kutua katika uwanja wa ndege wa Ciampino mjini Roma, saa kumi na mbili za jioni.
Akiwa agani alipeleka salaam za matashi mema kwa Rais a Kila taifa alilopita, ambayo ni
Korea China Mongolia Urusi Belarus Poland Slovakia Austria Slovenia Croatia Italia
Kwa Rais w Korea alisema, Mheshimwia Rais Park Guen-hye , Mimi sasa naondoka Korea kuelekea Roma, Kwa mara ingine narudia kutoa matashi yangu mema kwako wewe Rais na kwa raia wote na ninawaombea baraka za Mungu kwenu nyote ajili ya Amani na ustawi wa Rai ya Korea.
Kwa Rais wa China amesema, Mheshimiwa Xi Jinping, Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, ninayo heshima ya kukujulisha kuwa narudi Roma baada ya ziara yangu Korea, napenda kurudia tena kwako Mheshimiwa na raia wote wa China, matashi mema na naomba Baraka ziwe kwako na nchi yote ya China.
Na akipita katika anga la Mongolia , alipeleka salaam kwa Rais Tsakhiagiin Elbegdorj wa Mongolia, na kusema, Mheshimiwa Rais naruka juu ya anga la nchi yako, nikitokea Korea. Napenda kurudia salaam zangu za matashi mema kwako wewe na raia wote wa Mongolia, nawahakikishia sala zangu kwa taifa la Mongolia.
Na nchini Urusi alisema , Mheshimiwa Rais Vladimir Putin, Rais wa Shirikisho la Urusi nikiruka juu ya Urusi kutoka ziara yangu ya kichungaji nchini Korea, napenda kurudia matashi yangu mema kwako na kwa raia wote , na ninawahakikishia maombi yangu kwa taifa lako. Maneno kama hayo pia ameyatoa kwa mataifa mengine alipita Bielorussia, Poland, Slovakia, Austria, Slovenia, Croatia , na nchini Italia alimwambia Rais
Giorgio Napolitano , kwamba narejea toka safari ndefu ya Korea , ambako nimekutana na waamini wengi na uwakilishi wa utawala mzuri wa kupendeza wa Korea ambako kuna ukuaji mzuri katika yote kiroho na kijamii. Na kwa furaha zote , napenda kutoa kwako wewe Mheshimiwa, salaam zangu za upendo na kukuhakikishia sala maalum kwa ajili ya mema yote na utulivu wa taifa zima la Italia, na kwa upendo mkuu nalipa Baraka zangu. .








All the contents on this site are copyrighted ©.