Ulaya yaombwa kusitisha madhulumu kwa Wakristo Iraki
Mkuu wa Kanisa katika Antokia ya Siria , Mwenye Heri Yossef III, ametoa ombi kwa
Ulaya izuie madhulumu yanayo endelezwa kwa Wakristo Iraki.
Taarifa inasema,
kile kinachoendelea katika jamii ndogo ya Kikristo katika eneo linalokaliwa na jamii
kubwa ya Waislamu, eneo la nyanda za Ninawi, ni sawa na wimbi la tsunami, au ni
janga la karne. Mwenye Heri Youssef III, Patriaki wa Antokia ya Shamu, ametoa kilio
chake kupitia gazeti la Kifaransa "Ouest France", ambamo ametoa maelezo mapya na ombi
la kidharura kwa nchi za Magharibi, kusitisha mauaji ya kikabila na kidini yanayo
fanywa na wapiganaji wa Kiislamu, wanajihadi ISIS na kusaidia jamii ya Kikristo wa
Iraq.
Patriaki wa Lebanon ametoa hoja hiyo, hasa kwa Umoja wa Ulaya, akiangalisha
kwa taifa la Ufaransa, ambalo analitaja lina jukumu muhimu, na kama wajibu wake
kusitisha ukiukwaji wa haki za binadamu na ubaguzi wa kutisha nchini Iraki. Anasema
Ulaya inapaswa kupeleka ujumbe wake katika eneo hili la Mediterranean. Vinginevyo
- anaonya - jamii ya Kikristo ya Iraq, Syria na Lebanon ambazo ni kati ya jumuiya
kongwe za Mashariki ya Kati, inaweza kweli kutoweka pamoja na utamaduni na urithi
wake wa milenia.
Pamoja na hilo, ameuomba umoja wa Ulaya, usitishe upelekaji
wa silaha kwa mfululizo kwa makundi wanajihadi nchini Syria na Iraq, na pia kwa makundi
kadhaa ya wastani wa upinzani katika Syria. Pia kuzingatia maamuzi yaliyofikiwa na
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa , kuchukua hatua za haraka ili kusaidia kupunguza
makali ya mazingira magumu zaidi kwa makundi ya watu wachache Iraq; ikiwemo uzingatiaji
wa azimio la kisheria la Bodi, ili kuhakikisha kurudi mara moja kwa usalama wale
wote walio lazimika kukimbia makazi yao na mali. Na pia ameomba kuongezwa kwa mara
mbili zaidi misaada ya kibinadamu, ukiwemo msaada wa kidharura wa wakimbizi nchi
jirani ya Syria.