2014-08-18 15:04:22

Maadhimisho ya miaka 250 ya mji wa St Loui(USA)


Baba Mtakatifu Francisco, kwa barua yake ya kitume ya Julai 26, 2014, amempeleka Kardinali Justin Francis Rigali, kuwa mjumbe wake maalum kwa ajili ya sherehe za kutimia miaka 250 , mji wa St Louis Marekani, maadhimisho yatakayofanyika rasmi, tarehe 24 Agosti 2014, kwa Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu jipya la Saint Louis (USA).

Barua ya Papa kumteua Kardinali Rigali, ilichapishwa tarehe 26 Julai na kunukuliwa na gazeti la Vatican L'Osservatore Romano, ikimtaja Kardinali Francis Justin Rigali, Askofu Mkuu mstaafu wa Philadelphia (USA), kuwa Mjumbe Maalum wa Baba Mtakatifu, katika Ibada ya Misa ya Ekaristi, iliyopangwa katika Kanisa Kuu mpya ya Saint. Louis (USA) Agosti 24, 2014, kwa nia ya maadhimisho ya miaka 250 ya mwanzilishi wa mji St Louis.
Wengine walioteuliwa kuandamana na Kardinali Rigali ni pamoja Mons Breier J. Henry, Paroko wa Parokia ya Malaika Raphael na pia Mwenyekiti wa Baraza la Makasisi Mons. Leykam John Jpia Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Kupaswa Habari na Mshauri katika Baraza la moja ya Makasisi.

Aidha Baba Mtakatifu Francisko, katika ukurasa wake wa Tweet @pontifex, ametoa ombi maalum kwa ajili ya Iraki, ambamo ameomba,” mbele ya ghasia na fujo nyingi Iraki , tudumu katika sala na ukarimu” .
Ujumbe wa Papa pia unatutaka kuandamana na Mjumbe wake nchini Iraki , Kardinali Fernado Filoni , ambaye kwa wakati huu anatembelea Baghdad. Jumapili aliweza kukutana na jumuiya mbalimbali za kidini katika eneo lililokumbwa vibaya na machafuko la Yazid, ghasia za utumiaji silaha zinazofanywa na wanamgambo wa Kiislamu wa serikali ya Kiislamu.
Taarifa inabaini, Mjumbe binafsi ya Baba Mtakatifu nchini Iraki , Kardinali Fernando Filoni, akifuatana na Patriaki Sako, Mjumbe wa Kitume Iraki, na Maaskofu wa ndani, walikutana na viongozi wa kisiasa wa Utawala wa Mkoa wa Kurdistan na kuwatembelea wakimbizi Wakristo, Yazidis na mikoa mingine, Duhok na Erbil.

Baada ya kusikia na kuona maafa na mateso ya familia nyingi ambazo ziliondoka katika vijiji vyao kuacha nyumba na mali zao, hususani katika Mosul, na eneo la uwanda wa Ninawi na Sinjar, wote wameungana na ombi lililotolewa na Patriaki wa Kaldayo ya Babilonia, kuitaka Jumuiya ya Kimataifa , na hasa kwa nchi na mashirika ya kimataifa yenye kuwa na mamlaka zaidi ya uwajibikaji wa kimaadili, kuingilia kati mara moja, na kufanikisha msaada wa ubinadamu wa kidharura, maji, chakula, dawa, huduma za afya, nk. Na tatu ni kutoa ulinzi wa kimataifa kwa vijiji hivi kwa kuhamasisha familia kwa kurudi majumbani mwao na kuendelea maisha yao ya kawaida kwa usalama na amani. Katika maeneo hayo, Kardinali amesema kote watu wanapiga ukelele wa kuomba msaada wa kusitishwa ghasia na wana hamu yakurudi makwao.








All the contents on this site are copyrighted ©.