2014-08-16 15:16:56

Utume wa walei una thamani kubwa katika maisha ya kanisa!


Hotuba ya Baba Mtakatifu Francisko kwa Viongozi wa Utume wa Walei, imetazama hasa thamani ya karama mbalimbali katika shughuli za kitume ambazo huimarisha maisha ya Kanisa nchini Korea. Amesema kwamba, karama hizi huonyesha kwa hakika, uwepo wa upendo wa Mungu katika miito na kwa wengine, ni ishara ya kuonekana ya uwepo wa Ufalme wa Mungu.

Lakini Papa alibainisha, ni tu iwapo ushuhuda utakuwa na furaha ya kuvuta wanaume na wanawake kwa Kristo; na kwamba furaha hiyo, ndipo inakuwa ni zawadi inayolisha maisha ya sala, tafakari kwa Neno la Mungu, maadhimisho ya sakramenti na maisha ya jamii. Papa ameeleza mtindo wa maisha, kulingana na viapo vya usafi wa moyo, umaskini na utii, unakuwa ni ushuhuda wa furaha kwa upendo wa Mungu, uliosimikwa imara juu ya mwamba wa huruma yake.

Katika mkutano huu wa walei, uliohudhuriwa na wajumbe wapatao 150, ulilenga zaidi katika historia ya kanisa nchini Korea. Papa amesema, Kanisa la Korea, lina utajiri mkubwa wa imani iliyoachwa na wahenga waamini ambao walikuwa ni Wakristo wa kawaida. Kanisa nchini Korea ni mrithi wa imani ya vizazi vya watu wa kawaida ambao waliweza kuendeleza upendo wa Yesu Kristo katika ushirika na Kanisa, licha ya uhaba wa makuhani na tishio la mateso makali.

Papa alirejea uthabiti wa imani ya Mwenye Heri Paulo Yun Ji-chung na mashahidi wengine waliotangazwa katika Ibada ya Misa Jumamosi hii, kwamba, wanawakilisha sura ya ajabu ya historia ya Kanisa. Wao walitoa ushuhuda wa imani si tu kwa njia ya mateso yao hadi kufa, lakini pia na maisha yao ya upendo yaliyo oonesha mshikamano miongoni mwao kama jamii ya Kikristo, na hivyo kuwa mfano wa upendo kwa jamii yote.

Papa aliendelea kusema leo kama siku zote, Kanisa linahitaji walei kuwa shahidi wa kuaminika, ili ukweli kuokoa wa Injili, uonekane katika misingi ya maisha ya kawaida katika kujenga familia ya binadamu katika umoja, haki na amani. Papa Francis anasema kuwa, Kanisa la Mungu, ni moja tu , ambamo kila Mkristo aliyebatizwa ana jukumu muhimu katika hija hii ya kiroho.

Aidha Papa aliangalisha katika zawadi ya vipaji mbalimbali kwa walei, waume kwa wake, katika kutimiza utume wao mbalimbali, akisema, ina maana ya kukuza utume wa Kanisa katika kuhakikisha kwamba, ujumbe wa Neno la Mungu, unajipenyeza na kukamilishwa kwa Roho wa Kristo, hadi ujio wa Ufalme wake.

Papa ameonyesha kutambua kwa namna ya pekee, jinsi kazi za vyama vingi vya walei , hushiriki moja kwa moja katika shughuli na huduma kwa ajili ya maskini na wahitaji, hasa waliotupwa pembezoni na jamii. Na kwamba imani husambaa zaidi kupitia mshikamano halisi wenye upendo na udugu kwa ndugu zetu wake kwa waume, bila y akujali tofauti za utamaduni na hali ya kijamii, kwa sababu katika Kristo "hakuna Mgiriki na Myahudi".

Hata hivyo Papa alionya kusaidia maskini ni jambo jema, lakini haitoshi. Ni vyema kuzidisha juhudi katika maendeleo ya binadamu, kwa lengo kwamba, ili kila mtu, mke kwa mme, aweza kujua ukweli kwamba, furaha ya maisha yanayotokana na hadhi ya kupata mkate wa kila siku, hutoka kwa Mungu mwenyewe.

Papa ameonyesha kutambua mchango wa thamani unaotolewa na wanawake Wakatoliki wa Korea utume wa Kanisa, kama mama wa familia, makatekista na walimu, na kwa kupitia huduma zingine mbalimbali. Alisisitiza umuhimu wa ushuhuda unao tolewa na familia za Kikristo. Amesema, wakati huu wa mgogoro wa maisha ya familia, jamii ya Kikristo, imeitwa kutoa msaada kwa wanandoa na familia katika kutimiza kazi yao katika Kanisa na jamii. Familia ni taasisi msingi katika jamii na shule ya kwanza kwa watoto kujifunza maadili ya ubinadamu na maadili ya kiroho, ambayo msingi wa wema, uadilifu na haki katika jamii zetu.

Papa ametoa wito kwa walei kuendelea kukuza katika jamii yao, malezi adilifu kupitia udumishaji wa taratibu za kutoa katekesi kwa ajili ya mwelekeo chanya wa kiroho na uwepo wa kishawishi kamili cha kichungaji na ufahamu wa kutambua vipaji na karama katika kulitumikia kanisa katika umoja na katika roho ya kimisionari. Papa amesema , mchango wa walei ni muhimu, hata kwa ajili ya uwepo wa kanisa, kata kwa siku za baadaye si nchini Korea tu lakini Asia yote katika kugawana zawadi za kiroho.










All the contents on this site are copyrighted ©.