Baraza la Maaskofu Katoliki Malta linawakumbusha vijana na wanafunzi ambao kwa sasa
wamemaliza pilika pilika na patashika nguo kuchanika kwa ajili ya mitihani na tayari
wanaanza likizo ya kipindi cha kiangazi kuhakikisha kwamba, wanatumia muda huu vyema
kwa ajili ya kuku ana kukomaa: kiroho, kimwili na kiutashi wakiwa pamoja na familia
zao.
Hiki si kipindi
cha kujirusha, kwani vijana wengi wamejikuta wakijichumia majanga binafsi, familia
na jamii katika ujumla wake kwa kutozingatia utu na maadili mema wakati wa likizo!
Hiki ni kipindi cha vishawishi vinavyopaswa kuratibiwa kwa kuwa na utashi thabiti.
Ujumbe wa Baraza la Maaskofu Katoliki Malta unawataka wazazi na walezi kuwa karibu
na vijana wao nyakati hizi za likizo ili kuwasaidia kukua na kukomaa barabara!
Likizo
ni kipindi ambacho kinatoa mwanya kwa vijana kukuza na kuendeleza ut una vipaji vyao,
kwa kutumia vyema uhuru binafsi na muda alionao. Ni wakati wa kukuza na kuendeleza
mahusiano bora ya kijamii kwa kutambua kwamba, wakati wa shule pengine vijana hawana
muda sana wa kukaa na ndugu, jamaa na marafiki zao. Ni kipindi cha kazi, vijana wajitume
kusaidia kazi za nyumbani, kwa kujenga na kudumisha mshikamano wa upendo na familia.
Ni kipindi cha vijana kukuza na kuimarisha imani kwa Kristo na Kanisa lake!
Kwa
vijana ambao walikuwa na visingizio vya kukosa muda wa kwenda Kanisa kutokana na kubwana
sana na masomo, likizo wajitahidi kushiriki hata katika Jumuiya ndogo ndogo za Kikristo,
si tu wakati ule watakapokuwa wanatafuta cheti ili kuandikisha ndoa au wanapojisikia
kuwa na fununu ya wito wa kipadre na maisha ya kitawa! Vijana tangu mwanzo wajifunze
utamaduni wa kuboresha maisha yao ya kiroho kwa njia ya: Neno la Mungu, Sakramenti
za Kanisa na matendo ya huruma, kama kielelezo cha imani katika matendo! Maaskofu
Katoliki kutoka Malta wanakazia mambo makuu matatu: Kazi, Familia na Mapumziko!
Baraza
la Maaskofu Katoliki Malta linasema, vijana wakati wa likizo wanaweza kusaidia kuchangia
gharama za maisha katika familia zao kwa kufanya kazi za muda pale inapowezekana.
Hiki ni kipindi cha mpito kutoka shule na kuingia katika ulimwengu wa kazi, vijana
wanapaswa kuheshimiwa na kuthaminiwa utu wao, kwa kupewa mshahara wa haki.
Familia
ziwe makini kuhakikisha kwamba, vijana hawa wanafanya kazi kadiri ya umri na uwezo
wao. Vijana wawe na muda wa kutosha kukaa pamoja na familia zao, hiki kiwe ni kipaumbele
cha kwanza kwa vijana wenyewe na wazazi wawe mstari wa kwanza kuonesha mfano na ushuhuda
wa maisha.
Likizo ni muda wa vijana kujichotea nguvu ili kupambana kikamilifu
na changamoto za maisha. Vijana wajifunze kutumia vizuri muda wao na kwamba, wawe
makini ili wajanja wachache wasije wakawatumbukiza katika nyanyaso na dhuluma mbali
mbali kwa kigezo cha kutaka kuwapatia fedha, kwani fedha inaweza kuzaa fedhea.
Vijana
wajiepushe na makundi ya watu waliokengeuka kimaadilina kiutu kwani wanaweza kujikuta
huko huko wanajifunza matumizi haramu ya dawa za kulevya na ukahaba.
Mwishoni,
Baraza la Maaskofu Katoliki Malta linawaalika vijana kujitahidi kutumia muda wao kwa
ajili ya kuwasaidia wahitaji, michezo ili kujenga afya ya roho na mwili, wajifunze
kuonesha ukarimu, utu wema na uwajibikaji. Kwa njia hii likizo itakuwa ni fursa kweli
kwa vijana kukua kiroho na kimwili.